Muziki
Njooni Enyi Watakatifu


20

Njooni Enyi Watakatifu

Kwa ujasiri

1. Njooni enyi Watakatifu;

Kwa moyo tembea.

Safari yaweza kuwa ngumu,

Neema yatosha.

Ni bora tuvumilie

Wasiwasi tuondoe;

Fanya hivi, mfurahi—

Ni shwari! Ni shwari!

2. Je, tulijutie fungu letu?

Si hivyo; ni sawa.

Je, tuitegemee thawabu,

Vitani twatega?

Dhamiria; jipe moyo.

Mungu wetu nasi yupo;

Punde itanenwa hivi—

Ni shwari! Ni shwari!

3. Tutayapata makao mapya,

Sayuni tufike,

Ambapo hatutasumbuliwa;

Baraka tupate.

Tutapaza nyimbo zetu

Kumsifu Mungu wetu;

Na tutasema zaidi—

Ni shwari! Ni shwari!

4. Na tukifa kabla ya kufika,

Hakika! Ni shwari!

Tutakuwa huru, bila shida,

Tuishi peponi!

Na kama tutakuwepo

Kuliona kimbilio

Tutaimba jinsi gani—

Ni shwari! Ni shwari!

Maandishi: William Clayton, 1814–1879

Muziki: Wimbo wenye asili ya Uingereza

Mafundisho na Maagano 61:36–39

Mafundisho na Maagano 59:1–4