Muziki
Asante Mungu kwa Nabii


11

Asante Mungu kwa Nabii

Kwa uchangamfu

1. Asante Mungu kwa nabii,

Kutuongoza hizi siku.

Asante kuleta injili,

Iongezayo ufahamu.

Asante kwa kila baraka,

Pia kwa ukarimu wako.

Twapenda kukutumikia

Na kuzitii amri zako.

2. Na shida zinapotuzonga,

Na kutisha amani yetu,

Matumaini hutujia,

Kwamba wokovu u karibu.

Hatuna mashaka kwa Mungu

Ni dhahiri toka zamani.

Hakika wataangamizwa

Waovu wapinga Sayuni.

3. Tutamsifu siku zote.

Rehema zake tutaimba,

Tufurahie injiliye,

Na mwangaza wenye uzima.

Ukamilifu wa milele

Watapewa waaminifu,

Wakanao injili hii

Furaha hawata fahamu.

Maandishi: William Fowler, 1830–1865

Muziki: Caroline Sheridan Norton, 1808–mnamo 1877

Mafundisho na Maagano 21:1–5

Mosia 2:41