Muziki
Je, Uliomba?


72

Je, Uliomba?

Kwa kutafakari

1. Ulipoamka leo,

Je, uliomba?

Katika jina la Kristo,

Kusihi upendeleo

Ili kulindwa?

[Chorus]

Jinsi sala hufariji!

Nuru huongezeka.

Punde ukiwa gizani,

Kumbuka sala.

2. Ulipopata hasira,

Je, uliomba?

Upewe neema, ndugu,

Wengine usihukumu,

Waliokosa?

[Chorus]

Jinsi sala hufariji!

Nuru huongezeka.

Punde ukiwa gizani,

Kumbuka sala.

3. Ulipopatwa na shida,

Je, uliomba?

Ulipojawa huzuni,

Malhamu ya Gileadi

Ulitafuta?

[Chorus]

Jinsi sala hufariji!

Nuru huongezeka.

Punde ukiwa gizani,

Kumbuka sala.

Maandishi: Mary A. Pepper Kidder, 1820–1905

Muziki: William O. Perkins, 1831–1902

Zaburi 5:3, 12

Marko 11:24–25