Muziki
Kuna Lolote Jema Nimefanya?


128

Kuna Lolote Jema Nimefanya?

Kwa uchangamfu

1. Kuna lolote jema nimefanya?

Kuna niliyemuinua?

Kuna mwenye dhiki niliyefariji?

La sivyo, nimekosa.

Niliondolea mtu vikwazo

Kwa kujitolea kwangu?

Walipata nusuri wachovu nao?

Walipoita, nilijibu?

[Chorus]

Amka, fanya zaidi

Ya kuota u mbinguni.

Tenda jema daima, utafurahia

Baraka za maadili.

2. Fursa za kazi zipo hata sasa,

Nafasi zatujia tele.

Chunga usipitwe, usihairishe,

Bali nenda kafanye.

Ni uadilifu mtu kutoa;

Upendo unathawabu.

Mtenda jema, yeye ni msaada.

Wema sio bure kwa Mungu.

[Chorus]

Amka, fanya zaidi

Ya kuota u mbinguni.

Tenda jema daima, utafurahia

Baraka za maadili.

Maandishi na muziki: Will L. Thompson, 1847–1909, yamebadilishwa

Yakobo 1:22, 27

Alma 9:28