Muziki
Nifuate


57

Nifuate

Kwa unyenyekevu

1. “Nifuate,” alisema.

Nyayo zake kufuata,

Tuwe pamoja naye tu

Mwana Mpendwa wa Mungu.

2. “Nifuate,” semi fupi,

Bali mwanga wa ukweli

Upo kwenye hili neno

Ili kuwatia moyo.

3. Je, yatosha tu kujua

Twapaswa kumfuata,

Kwenye bonde la machozi?

La hasha, hata mbinguni.

4. Siyo tu kumfuata

Tukiwa kwenye dunia,

Hata tukiwekwa huru

Na Bwana turithi mbingu.

5. Ni lazima kuisaka

Njia ya kuendelea

Kumtafuta Mwokozi

Katika yoyote hali.

6. Enzi, himaya na nguvu,

Na utukufu ni vyetu,

Tukilitii milele,

Neno lake, “Nifuate.”

Maandishi: John Nicholson, 1839–1909

Muziki: Samuel McBurney, 1847–1909

Mathayo 4:19

2 Nefi 31:10–21