Muziki
Bwana Tunakuomba


83

Bwana Tunakuomba

Kwa sala

1. Bwana tunakuomba,

Bariki mafundisho

Na kwa kila mmoja

Yabaki mpaka mwisho.

2. Wakati wa ujana,

Tutafuata amri.

Utuongoze vyema,

Tupe nguvu tutii.

3. Baba mwenye huruma,

Tutafutapo haki,

Utujaze furaha

Tunapofanya kazi.

4. Tusamehe makosa;

Epusha vishawishi.

Ndipo tuishi vyema

Kitukufu mbinguni.

Maandishi: George Manwaring, 1854–1889

Muziki: Benjamin Milgrove, 1731–1810; umepangwa na Ebenezer Beesley, 1840–1906

Zaburi 119:33–35