121
Nilisikia Kengele
Kwa kutafakari
1. Nilisikia kengele,
Zikilia pande zote,
Nyimbo zao za upendo:
“Amani kwa watu wote.”
2. Niliwazia kengele
Zililia siku ile
Nyimbo nzuri za Krismasi:
“Amani kwa watu wote.”
3. Nilihisi kufa moyo,
Amani kutokuwepo,
Dunia inakejeli:
“Amani kwa watu wote.”
4. Nyimbo zikanikumbusha:
Mungu yupo, hajalala,
Haki itatushindia,
“Amani kwa watu wote.”
5. Nyimbo ziliendelea,
Usiku hadi mchana,
Kwa sauti ya ahadi:
“Amani kwa watu wote.”
Maandishi: Henry Wadsworth Longfellow, 1807–1882
Muziki: John Baptiste Calkin, 1827–1905
Luka 2:14