Muziki
Bwana Ni Mwokozi


27

Bwana Ni Mwokozi

Kwa shauku

1. Bwana ni Mwokozi

Na Mfalme wenu!

Mshangilieni

Na kumuabudu.

[Chorus]

Msifuni! Shangilia

Mkiimba kwa furaha!

Msifuni! Shangilia

Mkiimba kwa furaha!

2. Kitini pa enzi,

Bwana atawala.

Mungu wa ukweli

Alituokoa.

[Chorus]

Msifuni! Shangilia

Mkiimba kwa furaha!

Msifuni! Shangilia

Mkiimba kwa furaha!

3. Alishinda Kristo

Kote kutawala,

Funguo za kifo

Bwana alipewa.

[Chorus]

Msifuni! Shangilia

Mkiimba kwa furaha!

Msifuni! Shangilia

Mkiimba kwa furaha!

Maandishi: Charles Wesley, 1707–1788

Muziki: Horatio Parker, 1863–1919

Wafilipi 4:4

Zaburi 32:11