Muziki
Mwokozi, Niongoze


52

Mwokozi, Niongoze

Kwa sala

1. Mwokozi, niongoze

Dhoruba niipite;

Mawimbi yanizonga,

Hatari zajificha.

Mwenye ramani zote,

Mwokozi, niongoze.

2. Kama mwana kwa mama,

Bahari watuliza;

Mawimbi yakutii

Usemapo “Amani!”

Nahodha na Mfalme,

Mwokozi, niongoze.

3. Niifikapo pwani,

Kufura kwa mawimbi

Kwatisha pumziko;

Naegamia kwako,

Nasikia wasema,

“Tulia; Naongoza.”

Maandishi: Edward Hopper, 1818–1888

Muziki: John Edgar Gould, 1822–1875

Marko 4:39–41

Zaburi 48:14