Muziki
Nitakwenda Utakako


154

Nitakwenda Utakako

Kwa kushangilia

1. Labda siyo kwenye milima

Wala penye tufani,

Labda siyo mbele ya vita

Bwana anihitaji.

Akiniita, kwa upole

Nipite njia mpya,

Nitajibu, Bwana, Mwaminifu:

Utakako, nitakwenda.

[Chorus]

Nitakwenda utakako, Bwana,

Milimani hata ng’ambo;

Nitasema utakacho, Bwana;

Nitakuwa utakavyo.

2. Labda leo kuna maneno

Natakiwa niseme;

Labda kwenye njia za dhambi

Yupo asumbukaye.

Mwokozi wangu, niongoze,

Njiani penye giza,

Ili nitangaze neno tamu;

Utakacho, nitasema.

[Chorus]

Nitakwenda utakako, Bwana,

Milimani hata ng’ambo;

Nitasema utakacho, Bwana;

Nitakuwa utakavyo.

3. Kuna mahali duni hasa

Huko kwa walimwengu

Pa kwenda kufanyia kazi

Kwa ajili ya Yesu.

Hivyo najikabidhi kwako,

Nikijua napendwa,

Hili nafanya kwa moyo wote:

Utakavyo, nitakuwa.

[Chorus]

Nitakwenda utakako, Bwana,

Milimani hata ng’ambo;

Nitasema utakacho, Bwana;

Nitakuwa utakavyo.

Maandishi: Mary Brown, 1856–1918

Muziki: Carrie E. Rounsefell, 1861–1930

1 Nefi 3:7

Mafundisho na Maagano 4:2