Maandiko Matakatifu
Mafundisho na Maagano 1


Mafundisho na Maagano

Sehemu ya 1

Ufunuo uliotolewa kupitia Joseph Smith Nabii, 1 Novemba 1831, wakati wa mkutano maalumu wa wazee wa Kanisa, uliofanyika Hiram, Ohio. Mafunuo mengi yalikuwa yamekwisha pokelewa kutoka kwa Bwana kabla ya wakati huu, na ukusanyaji kwa ajili ya uchapishaji katika muundo wa kitabu ni moja ya mambo muhimu yaliyopitishwa katika mkutano huo. Sehemu hii inafanya utangulizi wa Bwana wa mafundisho, maagano, na amri alizozitoa katika kipindi hiki.

1–7, Sauti ya onyo ni kwa watu wote; 8–16, Ukengeufu na uovu utatangulia Ujio wa Pili; 17–23, Joseph Smith ameitwa kurejesha duniani ukweli na uwezo wa Bwana; 24–33, Kitabu cha Mormoni kinafichuliwa na Kanisa la kweli linaanzishwa; 34–36, Amani itaondolewa duniani; 37–39, Zichunguzeni amri hizi.

1 Sikilizeni, Enyi watu wa akanisa langu, yasema sauti ya yeye akaaye juu, na ambaye bmacho yake yako juu ya watu wote; ndiyo, amini ninawaambia: cSikilizeni enyi watu wa kutoka mbali; nanyi mlio juu ya visiwa vya bahari, sikilizeni kwa pamoja.

2 Kwani hakika asauti ya Bwana ni kwa watu wote, na bhakuna atakayeepuka; na hakuna jicho ambalo halitaona, wala sikio ambalo halitasikia, wala cmoyo ambao hautapenywa.

3 Na awaasi watachomwa kwa uchungu mwingi; kwani uovu wao butasemwa juu ya paa za nyumba, na matendo yao ya siri yatafichuliwa.

4 Na asauti ya onyo itakuwa kwa watu wote, kwa vinywa vya wanafunzi wangu, ambao nimewachagua katika bsiku hizi za mwisho.

5 Nao watasonga mbele wala hakuna wa kuwazuia, kwani Mimi Bwana nimewaamuru.

6 Tazama, hii ni amamlaka yangu, na ni mamlaka ya watumishi wangu, na ni utangulizi wa kitabu cha amri zangu, ambazo nimewapa wao bkuchapisha kwa ajili yenu, Enyi wakazi wa dunia.

7 Hivyo basi, aogopeni na tetemekeni, Enyi watu, kwani Mimi Bwana niliyoagiza ndani yake byatakamilika.

8 Na amini ninawaambia ninyi, kwamba wao waendeleao mbele, wakitangaza habari hizi kwa wakazi wa dunia, kwao uwezo umetolewa wa akufunga kote duniani na mbinguni, wale wasioamini na bwaasi;

9 Ndiyo, amini, kuwafungia wao hadi siku ile wakati aghadhabu ya Mungu itakapomwagwa juu ya bwaovu pasipo kipimo—

10 Hadi asiku ile wakati Bwana atakapokuja bkumlipa kila mtu kulingana na cmatendo yake, na dkumpimia kila mtu kulingana na kipimo alichowapimia wanadamu wenzake.

11 Kwa hiyo sauti ya Bwana ni hata miisho ya dunia, kwamba wale wote watakaosikia na wasikie:

12 Jitayarisheni, jitayarisheni kwa lile ambalo laja, kwani Bwana yu karibu;

13 Na ahasira ya Bwana inawaka, na bupanga wake unaoshwa mbinguni, nao utawashukia wakazi wa dunia.

14 Na amkono wa Bwana utafunuliwa; na siku yaja kwamba wale ambao bhawataisikia sauti ya Bwana, wala sauti ya watumishi wake, wala ckutii maneno ya manabii na mitume, dwatakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu;

15 Kwani awamepotoka kutoka kwenye bibada zangu, na cwamevunja dagano langu lisilo na mwisho;

16 aHawamtakii Bwana kuendeleza haki zake, bali kila mtu huenenda katika bnjia zake cmwenyewe, na akifuata dmfano wa mungu wake mwenyewe, ambaye ni mfano wa kitu cha duniani, na wa sanamu ya kuchonga, ambayo mali ghafi yake ehuzeeka na kuangamia katika fBabiloni, hata Babiloni ile kuu, ambayo itaanguka.

17 Hivyo basi, Mimi Bwana, nikijua majanga yajayo juu ya awakazi wa dunia, nimemwita mtumishi wangu Joseph Smith, Mdogo, na kusema naye kutoka mbinguni, na nikampa yeye amri;

18 Na pia nikawapa amri wengine, kwamba yawalazimu kuyatangaza mambo haya duniani; na haya yote kwamba yapate kukamilika yale yaliyoandikwa na manabii—

19 Mambo adhaifu ya dunia yatakuja kuyavunja yale yaliyo makubwa na yenye nguvu, kwamba mwanadamu asimshauri mwanadamu mwenzake, wala basiutegemee mkono wa mwanadamu—

20 Bali kwamba kila mwanadamu aweze akuongea katika jina la Mungu Bwana, hata Mwokozi wa ulimwengu;

21 Kwamba imani pia ipate kuongezeka katika dunia;

22 Kwamba aagano langu lisilo na mwisho liweze kuanzishwa;

23 Kwamba utimilifu wa ainjili yangu uweze bkutangazwa na watu walio cdhaifu na wa kawaida hata mwisho wa dunia, na mbele ya wafalme na watawala.

24 Tazama, Mimi ni Mungu; na nimeyasema haya; aamri hizi ni zangu, na zilitolewa kwa watumishi wangu katika udhaifu wao, kwa namna ya blugha yao, kwamba wapate ckuelewa.

25 Na hata wakikosea iweze kujulikana;

26 Na kadiri watakavyoitafuta ahekima waweze kuelekezwa;

27 Na kadiri walivyotenda dhambi waweze akukemewa, ili waweze bkutubu;

28 Na kadiri walivyokuwa awanyenyekevu waweze kufanywa imara, na kubarikiwa kutoka juu na kupokea bmaarifa mara kwa mara.

29 Baada ya kupokea kumbukumbu ya Wanefi, ndiyo, hata, mtumishi wangu Joseph Smith, Mdogo, kupata uwezo wa kutafsiri, Kitabu cha Mormoni, kwa rehema ya Mungu, na kwa uwezo wa Mungu, aKitabu cha Mormoni.

30 Na pia kwa wale ambao amri hizi zimetolewa, waweze kupata auwezo wa kuweka msingi wa bkanisa hili, na kulitoa kutoka lisikoonekana na kutoka cgizani, dkanisa pekee la kweli na lililo hai katika uso wa dunia yote, ambalo Mimi, Bwana, enapendezwa nalo, nikizungumza na kanisa kwa ujumla na siyo mmoja mmoja—

31 Kwani Mimi Bwana siwezi kuiangalia adhambi na kuivumilia hata kidogo;

32 Hata hivyo, yeye anayetubu na kutimiza amri za Bwana huyo aatasamehewa;

33 Na yeye ambaye ahatubu, kutoka kwake bitachukuliwa hata ile nuru aliyoipokea; kwani cRoho yangu dhaitashindana daima na mwanadamu, asema Bwana wa Majeshi.

34 Na tena, amini ninawaambia, Enyi wakazi wa dunia: Mimi Bwana ni radhi kufanya mambo haya yajulikane kwa watu awote;

35 Kwani asiwapendelei watu, na ninataka watu wote wajue kwamba bsiku ile yaja haraka; saa ingali, lakini i karibu, wakati camani itakapoondolewa duniani, na dibilisi atakuwa na uwezo juu ya utawala wake mwenyewe.

36 Na pia Bwana atakuwa na uwezo juu ya awatakatifu wake, naye batatawala ckatikati yao, na atashuka chini kwa dhukumu juu ya eIdumaya, au ulimwengu.

37 Zichunguzeni aamri hizi, kwani ni za kweli na za kuaminika, na unabii na bahadi zilizomo ndani yake zote zitatimilizwa.

38 Kile ambacho Mimi Bwana nimesema, nimekisema, na wala sijutii, na ingawa mbingu na dunia zitapita, aneno langu halitapita kamwe, bali blitatimia, iwe kwa csauti yangu mwenyewe au kwa sauti ya dwatumishi wangu, yote ni esawa.

39 Kwani tazama, na lo, Bwana ni Mungu, na aRoho hushuhudia, na ushuhuda wake ni wa kweli, na bukweli hudumu milele na milele. Amina.