Maandiko Matakatifu
Mafundisho na Maagano 80


Sehemu ya 80

Ufunuo uliotolewa kupitia Joseph Smith Nabii, kwenda kwa Stephen Burnett, Hiram, Ohio, 7 Machi 1832.

1–5, Stephen Burnett na Eden Smith wanaitwa kuhubiri katika mahali popote watakapochagua.

1 Amini, hivyo ndivyo asemavyo Bwana kwako wewe mtumishi wangu Stephen Burnett: Nenda wewe, nenda wewe ulimwenguni na aukahubiri injili kwa kila kiumbe kitakachokuwa chini ya sauti yako.

2 Na kwa vile unataka mwenza, nitakupa mtumishi wangu Eden Smith.

3 Kwa hiyo, nendeni na mkaihubiri injili yangu, iwe kaskazini au kusini, mashariki au magharibi, si kitu, kwani hamwezi kukosea.

4 Kwa sababu hiyo, yatangazeni mambo ambayo mmeyasikia, na hakika kuyaamini, na akujua ni ya kweli.

5 Tazama, haya ndiyo mapenzi yake yeye aaliyewaita ninyi, Mkombozi wenu, hata Yesu Kristo. Amina.