Maandiko Matakatifu
Mafundisho na Maagano 31


Sehemu ya 31

Ufunuo uliotolewa kupitia Joseph Smith Nabii kwa Thomas B. Marsh, Septemba 1830. Tukio hili lilitokea muda mfupi baada ya mkutano wa Kanisa (ona kichwa cha habari cha sehemu ya 30). Thomas B. Marsh alikuwa amebatizwa mwanzoni mwa mwezi huo na kutawazwa kuwa mzee katika Kanisa kabla ya kutolewa kwa ufunuo huu.

1–6, Thomas B. Marsh ameitwa kuihubiri injili na anahakikishiwa ustawi wa familia yake; 7–13, Anashauriwa kuwa mvumilivu, kusali daima, na kumtii Mfariji.

1 aThomas, mwanangu, umebarikiwa kwa sababu ya imani yako katika kazi yangu.

2 Tazama, umepata mateso mengi kwa sababu ya familia yako; hata hivyo, nitakubariki wewe na familia yako, ndiyo, watoto wako; na siku yaja ambayo wataamini na kujua ukweli na kuwa pamoja na wewe katika kanisa langu.

3 Inua moyo wako na ufurahi, kwani saa ya huduma yako imewadia; na ulimi wako utalegezwa, nawe utatangaza habari anjema ya shangwe kuu kwa kizazi hiki.

4 aUtatangaza mambo yale ambayo yamefunuliwa kwa mtumishi wangu, Joseph Smith, Mdogo. Utaanza kuhubiri kutoka wakati huu, ndiyo, kuvuna katika shamba ambalo ni bjeupe lililo tayari kuchomwa.

5 Kwa hiyo, aingiza mundu yako kwa moyo wako wote, na dhambi zako bzitasamehewa, na wewe utachukua cmiganda mgongoni mwako, kwani dmtenda kazi amestahili ujira wake. Kwa hivyo, familia yako itaishi.

6 Tazama, amini ninakuambia, enenda kutoka kwao japo kwa wakati mfupi, na utangaze neno langu, na Mimi nitawatayarishia mahali.

7 Ndiyo, anitaifungua mioyo ya watu, nao watakupokea. Nami nitalianzisha kanisa kwa mkono wako;

8 Nawe autawaimarisha na kuwatayarisha kwa ajili ya wakati watakapo kusanyika.

9 Uwe amvumilivu wakati wa bmateso, usiwashutumu wenye kukushutumu. Itawale cnyumba yako kwa unyenyekevu, na uwe thabiti.

10 Tazama, ninakuambia kwamba utakuwa tabibu kwa kanisa, bali siyo kwa walimwengu, kwani wao hawatakupokea.

11 Nenda zako kokote nitakakokutuma, na utapewa na aMfariji, lile la kufanya na mahali pa kwenda.

12 aOmba daima, usije ukaanguka bmajaribuni na kupoteza thawabu yako.

13 Uwe amwaminifu hata mwisho, na lo, Mimi ni bpamoja nawe. Maneno haya siyo ya mwanadamu wala ya wanadamu, bali yangu Mimi, Yesu Kristo, Mkombozi wako, kwa cmapenzi ya Baba. Amina.