Maandiko Matakatifu
Mafundisho na Maagano 6


Sehemu ya 6

Ufunuo uliotolewa kwa Joseph Smith Nabii na Oliver Cowdery, huko Harmony, Pennsylvania, Aprili 1829. Oliver Cowdery alianza kazi yake ya uandishi katika tafsiri ya Kitabu cha Mormoni, 7 Aprili 1829. Alikuwa tayari amekwisha pokea ufunuo mtakatifu wa ukweli wa ushuhuda wa Nabii kuhusiana na mabamba ambayo juu yake imechorwa kumbukumbu ya Kitabu cha Mormoni. Nabii alimwuliza Bwana kupitia Urimu na Thumimu naye akapata jibu hili.

1–6, Wafanyakazi katika shamba la Bwana hupata wokovu; 7–13, Hakuna zawadi iliyo kubwa zaidi kuliko zawadi ya wokovu; 14–27, Ushuhuda wa ukweli huja kwa uwezo wa Roho; 28–37, Mtegemee Kristo na tenda mema daima.

1 Kazi kubwa na ya aajabu i karibu kuja kwa wanadamu.

2 Tazama, Mimi ndimi Mungu; litiini aneno langu, lililo hai na lenye nguvu, bkali kuliko upanga wenye makali pande mbili, kwa kugawanya viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; hivyo basi yatiini maneno yangu.

3 Tazama, ashamba ni jeupe tayari kwa mavuno; kwa hiyo, yeyote atakaye kuvuna, na aingize mundu yake kwa nguvu zake, na kuvuna wakati siku ingali, ili aweze kujiwekea akiba kwa ajili ya nafsi yake wokovu usio na mwisho katika ufalme wa Mungu.

4 Ndiyo, yeyote yule aatakayeingiza mundu yake na kuvuna, yeye huyo ameitwa na Mungu.

5 Kwa hiyo, kama wewe autaniomba mimi utapata, kama utabisha utafunguliwa.

6 Sasa, kama ulivyoomba, tazama ninakuambia, shika amri zangu, na atafuta kuianzisha na kustawisha kusudi la bSayuni;

7 aUsitafute butajiri bali chekima, na tazama, dsiri za Mungu zitafichuliwa kwako, na ndipo wewe utafanywa tajiri. Tazama, yeye aliye na euzima wa milele ndiye tajiri.

8 Amini, amini, nakuambia, kama unavyotaka kwangu na itakuwa hivyo kwako; na kama unataka, utakuwa chanzo cha kufanya mambo mema mengi katika kizazi hiki.

9 Usiseme lolote bali atoba kwa kizazi hiki; shika amri zangu, na saidia kuitenda kazi yangu, kulingana na amri zangu, na wewe utabarikiwa.

10 Tazama nawe unacho kipawa, na umebarikiwa kwa sababu ya kipawa chako. Kumbuka ni akitakatifu na chatoka juu—

11 Na kama wewe autauliza, utapata kujua bsiri zilizo kubwa na za ajabu; hivyo basi wewe unapaswa kutumia ckipawa chako, kwamba uweze kuzigundua siri, kwamba uweze kuwaleta wengi kwenye maarifa ya ukweli, ndiyo, dkuwashawishi wao juu ya makosa ya njia zao.

12 Usifanye kipawa chako kijulikane kwa yeyote ila kwa wale tu wa imani yako. Usicheze na mambo amatakatifu.

13 Kama wewe wataka kutenda mema, ndiyo, na aendelea kwa buaminifu hadi cmwisho, nawe utaokolewa katika ufalme wa Mungu, ambayo ndiyo zawadi kubwa kuliko zote kwa Mungu; kwani hakuna zawadi kubwa zaidi kuliko zawadi ya dwokovu.

14 Amini, amini, nakuambia, umebarikiwa wewe, kwa kile ulichofanya; kwani wewe aumeniuliza Mimi, na tazama, kama daima ulivyoniuliza, nawe umepata maelekezo ya Roho wangu. Kama isingelikuwa hivyo, wewe usingelifika mahali ulipo sasa.

15 Tazama, na wewe wajua kwamba uliniuliza Mimi na Mimi nikaiangaza aakili yako; na sasa ninakuambia wewe mambo haya kwamba uweze kuelewa kwamba wewe uliangaziwa na Roho wa ukweli;

16 Ndiyo, ninakuambia, ili wewe upate kujua kwamba hapana yeyote ila Mungu ambaye ahujua mawazo yako na dhamira ya bmoyo wako.

17 Ninakuambia mambo haya kama ushahidi kwako—kwamba maneno au kazi ambayo wewe umekuwa ukiandika ni ya akweli.

18 Kwa hivyo fanya abidii; bsimama pamoja na mtumishi wangu Joseph, kiuaminifu, katika hali yoyote iwayo ngumu atakayoweza kuwa kwa sababu ya neno.

19 Muonye katika makosa yake na pia pokea maonyo yake. Kuwa mvumilivu; mtulivu; mwenye kiasi, uwe na subira, imani, tumaini na hisani.

20 Tazama, wewe ndiwe Oliver, na nimesema nawe kwa sababu ya matakwa yako; kwa hiyo ayatunze maneno haya katika moyo wako. Uwe mwaminifu na mwenye juhudi katika kushika amri za Mungu, na mimi nitakuzungushia mikono ya upendo wangu.

21 Tazama, Mimi ndimi Yesu Kristo, aMwana wa Mungu. Mimi ni yule yule ambaye nilikuja kwa walio bwangu, na walio wangu hawakunipokea. Mimi ni cnuru inayongʼaa dgizani, nalo giza halikuiweza.

22 Amini, amini, ninakuambia, kama wataka ushahidi zaidi, rejesha mawazo yako juu ya usiku ule uliponililia katika moyo wako, kwamba uweze akujua ukweli wa mambo haya.

23 Sikusema aamani akilini mwako kuhusiana na jambo hili? Ni bushahidi gani mkubwa zaidi unaoweza kupata kuliko kutoka kwa Mungu?

24 Na sasa, tazama, umepata ushahidi; kwani kama mimi nimekuambia mambo ambayo hakuna mtu ajuaye, je hujapata ushahidi?

25 Na, tazama, ninakupa kipawa, kama wataka kutoka kwangu, cha akutafsiri, hata kama mtumishi wangu Joseph.

26 Amini, amini, ninakuambia, kwamba zipo akumbukumbu ambazo zimechukua kiasi kikubwa cha injili yangu, ambayo ilizuiliwa kwa sababu ya buovu wa watu;

27 Na sasa ninakuamuru, kwamba kama unayo tamaa njema—tamaa ya kujiwekea hazina yako mbinguni—ndipo utasaidia katika kuzileta kwenye nuru, kwa kipawa chako, sehemu zile za amaandiko yangu matakatifu ambayo yamefichwa kwa sababu ya uovu.

28 Na sasa, tazama, ninakupa wewe pamoja na mtumishi wangu Joseph funguo za kipawa hiki, ambacho kitaileta nuruni huduma hii; na katika vinywa vya amashahidi wawili au watatu kila neno lithibitike.

29 Amini, amini, ninawaambia, kama wao wanakataa maneno yangu, na sehemu hii ya injili yangu na huduma, mmebarikiwa ninyi, kwani wao hawatafanya zaidi kwenu kuliko walivyonifanyia mimi.

30 Na hata kama awatawafanyia ninyi kama walivyonifanyia Mimi, mmebarikiwa ninyi, kwani bmtaishi pamoja na mimi katika cutukufu.

31 Lakini kama ahawatayakataa maneno yangu, ambayo yataanzishwa kwa bushuhuda ambao utatolewa, wamebarikiwa wao, na ndipo ninyi mtapata shangwe ya matunda ya kazi yenu.

32 Amini, amini, ninawaambia, kama nilivyosema kwa wanafunzi wangu, walipo wawili au watatu awaliokusanyika pamoja katika jina langu, wakigusia jambo moja, tazama, mimi nitakuwa bkatikati yao—hata sasa nipo katikati yenu.

33 aMsiogope kufanya mema, wana wangu, kwani chochote bunachopanda, ndicho pia wewe utakachokivuna; kwa hiyo kama utapanda mema pia utavuna mema kwa thawabu zenu.

34 Kwa sababu hiyo, msiogope, enyi kundi dogo; tendeni mema; acha dunia na jehanamu ziungane dhidi yenu, kwani kama mmejengwa juu ya amwamba wangu, haziwezi kuwashinda.

35 Tazama, siwahukumu ninyi; nendeni zenu na msitende adhambi tena; fanyeni kwa utaratibu kazi ambayo nimewaamuru.

36 aNitegemeeni katika kila wazo; msitie shaka, msiogope.

37 aTazama majeraha yaliyoko yaliotobolewa ubavuni mwangu, na pia alama za bmisumari katika mikono na miguu yangu; kuweni waaminifu, zishikeni amri zangu, na cmtaurithi dufalme wa mbinguni. Amina.