Maandiko Matakatifu
Mafundisho na Maagano 68


Sehemu ya 68

Ufunuo uliotolewa kupitia Joseph Smith Nabii, huko Hiram, Ohio, 1 Novemba 1831, katika jibu la maombi kwamba mapenzi ya Bwana yafahamike kuhusu Orson Hyde, Luke S. Johnson, Lyman E. Johnson, na William E. McLellin. Ingawa sehemu ya ufunuo huu ilielekezwa kwa watu hawa wanne, mengi ya yaliyomo yanalihusu Kanisa zima. Ufunuo huu ulipanuliwa kwa maelekezo ya Joseph Smith wakati ulipochapishwa katika toleo la mwaka 1835 la Mafundisho na Maagano.

1–5, Maneno ya wazee wakati wakiongozwa na Roho Mtakatifu ni maandiko; 6–12, Wazee watahubiri na kubatiza, na ishara zitawafuata waumini wa kweli; 13–24, Mzaliwa wa kwanza miongoni mwa wana wa Haruni aweza kutumika kama Askofu Kiongozi (hii maana yake, anashikilia funguo za urais kama askofu) chini ya maelekezo ya Urais wa Kwanza; 25–28, Wazazi wanaamriwa kuwafundisha injili watoto wao; 29–35, Watakatifu wataishika Sabato, watafanya kazi kwa bidii, na kuomba.

1 Mtumishi wangu, Orson Hyde, aliitwa kwa kutawazwa kwake kuitangaza injili isiyo na mwisho, kwa aRoho wa Mungu aliye hai, kutoka taifa hadi taifa, na kutoka nchi hadi nchi, katika mikutano ya waovu, katika masinagogi yao, akisemezana nao na kuwaelezea maandiko yote.

2 Na, tazama, na lo, huu ni mfano kwa wale wote ambao wametawazwa katika ukuhani huu, wale ambao kazi imekwisha tolewa kwao kwenda—

3 Na huu ni mfano kwao, kwamba awatasema kama vile walivyoongozwa na Roho Mtakatifu.

4 Na lolote watakalolisema wakati wanaongozwa na aRoho Mtakatifu litakuwa andiko, litakuwa ni mapenzi ya Bwana, litakuwa ni nia ya Bwana, litakuwa ni neno la Bwana, itakuwa ni sauti ya Bwana, na ni buwezo wa Mungu kwa wokovu.

5 Tazama, hii ni ahadi ya Bwana kwenu, Enyi watumishi wangu.

6 Kwa hiyo, changamkeni, na amsiogope, kwani Mimi Bwana nipo pamoja nanyi, na nitasimama karibu yenu; nanyi mtanishuhudia, hata Yesu Kristo, kuwa Mimi ndimi Mwana wa Mungu aliye hai, kwamba nilikuwepo, kwamba nipo, na kwamba nitakuja.

7 Hili ndilo neno la Bwana kwenu, mtumishi wangu aOrson Hyde, na pia mtumishi wangu Luke Johnson, na kwa mtumishi wangu Lyman Johnson, na kwa mtumishi wangu William E. McLellin, na kwa wazee wote waaminifu wa kanisa langu—

8 aEnendeni ulimwenguni mwote, bmkaihubiri injili kwa kila ckiumbe, mkitenda katika dmamlaka ambayo nimewapa, emkibatiza katika jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.

9 Na ayule aaminiye na kubatizwa bataokolewa, na yule asiyeamini catalaaniwa.

10 Na yule aliyeamini atabarikiwa kwa aishara kumfuata, hata kama ilivyoandikwa.

11 Nanyi mtapewa kujua aishara za nyakati, na ishara za kuja kwa Mwana wa Mtu;

12 Na kuhusu wale wote kama vile Baba atakavyowashuhudia, ninyi mtapewa uwezo wa akuwafunga katika uzima wa milele. Amina.

13 Na sasa, kuhusu mambo ya nyongeza katika maangano na amri, nayo ni haya—

14 Yanayobaki baada ya hapa, katika wakati wa Bwana ufikapo, amaaskofu wengine wateuliwe kwa ajili ya kanisa, kuhudumu hata kama wale wa kwanza;

15 Kwa hiyo, watakuwa amakuhani wakuu wenye kustahili, na wateuliwe na bUrais wa Kwanza wa Ukuhani wa Melkizedeki, isipokuwa wale walio wazaliwa wa ukoo wa cHaruni.

16 Na kama watakuwa wazaliwa halisi wa ukoo wa aHaruni wao wanayo haki kisheria ya uaskofu, kama ni wazaliwa wa kwanza miongoni mwa wana wa Haruni;

17 Kwani mzaliwa wa kwanza anashikilia haki ya urais wa Ukuhani huu, na afunguo au mamlaka yake.

18 Hakuna mtu aliye na haki kisheria kwenye ofisi hii, kushikilia funguo za ukuhani huu, isipokuwa yule aliye amzaliwa halisi wa ukoo na ni mzaliwa wa kwanza wa Haruni.

19 Lakini, kama akuhani mkuu wa Ukuhani wa Melkizedeki anayo mamlaka ya kutenda katika ofisi zile ndogo anazoweza kuzitenda kazi katika ofisi ya baskofu ikiwa hakuna mzaliwa halisi wa ukoo wa Haruni anayeweza kupatikana, ili mradi ameitwa na kutengwa na kutawazwa katika mamlaka haya, chini ya mikono ya Urais wa Kwanza wa Ukuhani wa Melkizedeki.

20 Na mzaliwa halisi wa ukoo wa Haruni, pia, lazima ateuliwe na Urais huu, na aonekane mwenye kustahili, na akupakwa mafuta, na bkutawazwa chini ya mikono ya Urais huu, vinginevyo hawajaruhusiwa kisheria kutenda kazi katika ukuhani wao.

21 Lakini, kwa sababu ya kupitia azimio kuhusu haki yao ya ukuhani kutoka kwa baba hadi kwa mwana, wanaweza kudai haki ya kupakwa kwao mafuta kama wakati wowote wanaweza kuthibitisha safu ya mfuatano wa kuzaliwa, au itafanywa kwa kuhakikisha kwa ufunuo kutoka kwa Bwana chini ya mikono ya Urais uliotajwa hapo juu.

22 Na tena, hakuna askofu au kuhani mkuu ambaye atasimikwa kwa ajili ya huduma hii ambaye atashtakiwa au kuhukumiwa kwa jinai yoyote, isipokuwa mbele ya aUrais wa Kwanza wa kanisa;

23 Na kadiri atapatikana na hatia mbele ya Urais huu, kwa ushuhuda ambao hauwezi kutuhumiwa, atahukumiwa;

24 Na kama atatubu aatasamehewa, kulingana na maagano na amri za kanisa.

25 Na tena, ili mradi awazazi wanao watoto katika Sayuni, au katika bkigingi chake chochote ambacho kimeundwa, ambao chawawafundishi wao kuelewa mafundisho ya toba, imani katika Kristo Mwana wa Mungu aliye hai, na ubatizo na kipawa cha Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono, wafikapo dmiaka minane, edhambi zao zitakuwa juu ya vichwa vya wazazi.

26 Kwani hii itakuwa sheria kwa wakazi wa aSayuni, au katika kila kigingi chake kilichoundwa.

27 Na watoto wao awabatizwe kwa ajili ya bondoleo la dhambi zao wafikishapo umri wa miaka cminane na kupokea kuwekwa mikono.

28 Na pia wawafundishe watoto wao akuomba, na kusimama wima mbele za Bwana.

29 Na wakazi wa Sayuni pia waikumbuke siku ya aSabato kuishika kitakatifu.

30 Na wakazi wa Sayuni pia wazikumbuke kazi zao, ili mradi wameteuliwa kufanya kazi, kwa uaminifu wote; kwani mvivu atakumbukwa mbele za Bwana.

31 Sasa, Mimi, Bwana sipendezwi na wakazi wa Sayuni, kwani kuna awavivu miongoni mwao; na watoto wao pia wanakua katika buovu; pia chawatafuti kwa dhati utajiri wa milele, bali macho yao yamejaa tamaa.

32 Mambo haya hayafai kuwa hivyo, na lazima yakomeshwe kutoka miongoni mwao; kwa hiyo, acha mtumishi wangu Oliver Cowdery ayapeleke maneno haya kwenye nchi ya Sayuni.

33 Na amri ninatoa kwao—kwamba yule asiyefanya asala zake mbele za Bwana katika wakati unaostahili, acha bakumbukwe mbele za mwamuzi wa watu wangu.

34 Na amisemo hii ni ya kweli na ya kuaminika; kwa hiyo, msiivunje, wala bkuondoa lolote ndani yake.

35 Tazama, Mimi ni aAlfa na Omega, na bnaja haraka. Amina.