Misaada ya Kujifunza
2. Mlima Sinai (Horebu) na Nyika za Sinai


2. Mlima Sinai (Horebu) na Nyika za Sinai

Picha
picha 2

Kuna maeneo kadhaa yanayowezekana kuwa ndiyo mahali pa Mlima Sinai. Moja ya maeneo ya kimapokeo ni Yebeli Musa (Mlima wa Musa), uliopigwa picha hapa.

Matukio Muhimu: Mungu alimtokea Musa na akampa Amri Kumi (Ku. 19–20). Musa, Haruni, wana wawili wa Haruni, na wazee 70 walimwona na kuzungumza na Mungu (Ku. 24:9–12). Mungu alimpa Musa maelekezo kwa ajili ya kujenga hema (Ku. 25–28; 30–31). Waisraeli walimwabudu ndama wa dhahabu ambaye walimshawishi Haruni kumtengeneza (Ku. 32:1–8). Eliya alikimbilia katika nchi hii kutoka Bonde la Yereezeli, mahali ambapo Malkia Yezebeli aliishi (1 Fal. 19:1–18). Hapa ni mahali ambapo pia Eliya alizungumza na Mungu (1 Fal. 19:8–19). (Ona MWM Sinai, Mlima.)