Rafiki
Shughuli ya Hadithi ya Familia
Ubatizo na Uthibitisho


“Shughuli ya Hadithi ya Familia,” Rafiki, Agosti 2023, 30–31.

Shughuli ya Hadithi ya Familia

“Je, unaweza kusimulia hadithi nyingine ya familia?” Lorrain aliuliza.

Hadithi hii ilitokea huko Vanuatu.

Lorrain alitabasamu alipokuwa anaimba maneno ya mwisho ya wimbo. Walikuwa punde tu wamemaliza wakati wa kuimba katika Msingi. Sasa ulikuwa ni wakati wa kwenda darasani.

Lakini kwanza, Dada Taleo alisimama. “Ninataka kuwaambia kuhusu shughuli ya Msingi ambayo inakuja hivi karibuni,” alisema. “Tunataka kila mmoja wenu ajifunze kuhusu familia yenu. Waulize wazazi wako kuhusu hadithi za familia. Kisha katika shughuli hii, kila mmoja wenu anaweza kushiriki kile alichojifunza.”

Wakati Lorrain alipofika nyumbani kutoka kanisani, alikuwa na msisimko. Alipata kipande kikubwa cha karatasi na kukipeleka mezani. Hakuweza kusubiri kujifunza kuhusu familia yake!

Lorrain alichora mti wa familia kwenye karatasi. Mama na Baba yake walimsaidia kuandika majina yote. Kisha aligundisha picha za wanafamilia yake kwenye bango.

Picha
alt text

“Jina la bibi wa mama yako lilikuwa Lorrain pia,” Mama alisema. “Tulikupa jina lake.”

“Wow,” Lorrain alisema.

“Bibi Lorrain alikuwa mtu mwenye upendo sana.” Mama alitabasamu. “Wakati watu wengine katika kijiji walipoishiwa kuni za kuwashia mioto yao, Bibi Lorrain alishiriki nao.”

Kujifunza kuhusu familia yake kuliburudisha zaidi! “Je, unaweza kusimulia hadithi nyingine ya familia?” Lorrain aliuliza.

“Baba angeweza kukuambia kuhusu mara ya kwanza yeye alipoenda hekaluni,” Mama alisema. “Alikuwa na umri wa miaka sita tu. Yeye na wazazi wake walifunga safari ndefu kuelekea hekaluni huko New Zealand.”

Lorrain alipenda kusikia kuhusu hekalu. “Nisimulie hadithi hiyo, Baba!” alisema.

“Kwanza tulipanda ndege kwenda New Zealand. Kisha tukasafiri kwa basi. Ilikuwa safari ndefu.” Baba alimwonyesha Lorrain picha ya hekalu. “Mwishowe mimi na wazazi wangu tuliingia ndani. Tuliunganishwa kama familia. Hiyo inamaanisha tunaweza kuwa pamoja milele!”

Hiyo ilimfurahisha Lorrain moyoni. Alifurahi kwamba aliweza kusikia hadithi kuhusu familia yake.

Mwishowe asubuhi ya shughuli ya Msingi ilifika. Lorrain alimsaidia Mama na Dada Taleo kutayarisha kila kitu katika jengo la kanisa.

Kisha walisikia habari fulani za kusisimua. Hekalu lingejengwa katika kisiwa chao!

Lorrain alikuwa na furaha sana. Atakapokuwa mkubwa vya kutosha kuingia ndani ya hekalu, hatahitaji kusafiri mbali tena!

Usiku huo, marafiki wote wa Lorrain walikuwa katika shughuli ya Msingi. Watoto walifanya zamu kushiriki kile walichojifunza kuhusu familia zao. Ilipofika zamu ya Lorrain, alinyanyua bango lake la mti wa familia yake.

“Nilivutiwa sana kujifunza kuhusu familia yangu,” alisema. “Nilijifunza kwamba mimi nilipewa jina la bibi wa mama yangu. Pia nilijifunza kuhusu mara ya kwanza familia yangu ilipokwenda hekaluni. Hekalu linaweza kusaidia familia yetu kuwa pamoja milele.” Hisia nzuri zilirudi tena. “Nilisisimka sana kwamba tutakuwa na hekalu hapa Vanuatu.”

Lorrain aliketi chini akiwa na tabasamu kubwa usoni mwake. Alikuwa na shukrani kwamba angeweza kukua zaidi kama Yesu. Na alikuwa mwenye shukrani kwa ajili ya hekalu! Alikuwa na shauku ya kuingia ndani siku moja.

Picha
alt text
Picha
alt text here

Vielelezo na Emily Davis