Rafiki
Yesu Alituonyesha Njia
Ubatizo na Uthibitisho


“Yesu Alituonyesha Njia,” Rafiki, Agosti 2023, 4– 4.

Yesu Alituonyesha Njia

Picha
Alt text

Kielelezo na Dan Burr

Yesu Kristo ni Mwana wa Baba wa Mbinguni. Yeye alikuja ulimwenguni kutuonyesha jinsi tunavyoweza kurudi kwa Baba wa Mbinguni siku moja. Yesu alibatizwa. Yeye alitufunza kwamba tunapaswa kubatizwa pia.

Picha
alt text

Yesu alituonyesha jinsi ya kuishi. Yeye alimpenda na kumsaidia kila mmoja. Yeye anatutaka tumfuate Yeye.

Picha
alt text

Yesu Kristo aliusikia uchungu wetu wote na aliteseka kwa ajili ya dhambi zetu. Kisha Yeye alikufa kwa ajili yetu. Huu unaitwa Upatanisho wa Yesu Kristo. Yeye alifufuka. Inamaanisha kwamba Yeye anaishi leo! Kwa sababu ya Yesu Kristo, sisi pia tutaishi tena baada ya kufa.

Picha
alt text

Yesu alifanya vitu hivi vyote kwa ajili yetu kwa sababu Yeye anatupenda. Kwa sababu Yake, sisi tunaweza kuishi mbinguni pamoja na familia zetu siku moja.

Picha
alt text

Tunaweza kumfuata Yesu kwa kubatizwa. Sisi pia tunaweza kumfuata Yeye kila siku tunapowapenda na kuwasaidia wengine na kutii amri Zake.