Rafiki
Jiwe la Zambarau lenye Kung’aa
Machi 2024


“Jiwe la Zambarau lenye Kung’aa,” Rafiki, March 2024, 10–11.

Jiwe la Zambarau lenye Kung’aa

Kama angesema ukweli, je, yeye angemkasirikia?

Hadithi hii ilitokea huko Uholanzi.

Marie alifungua sanduku lake la kutunzia kidani ili kutazama mawe yake mazuri. Moja baada ya jingine, aliyashikilia mkononi mwake. Moja jekundu, kisha la kijani, kisha jeupe sana.

Bibi aligonga mlango wa chumba chake cha kulala. “Uko tayari kuondoka?”

“Ndiyo!” Marie kwa makini aliyaweka mawe tena katika sanduku lake.

Bibi alikuwa anampeleka Marie kwenye maktaba. Lakini siyo tu kutanzama vitabu. Kulikuwa na maonyesho ya jiwe maalumu huko! Marie alikuwa na shauku.

Wakati basi lao lilipofika kwenye maktaba, Marie na Bibi walitembea kuingia ndani. Wakaona meza na meza zenye mawe mazuri sana. Mengine yalikuwa yanag’aa na laini. Mengine yalikuwa na maumbo ya kupendeza.

“Angalia hili! Bibi alionesha kwa kidole fuwele kubwa. Lilikuwa na miiba ya samawati iliyochomoza kila mahali.

Meza nyingine ilikuwa na mawe mengi madogo, ya mviringo. Marie aliangalia rangi zote. Na mwishoni kabisa kulikuwa na jiwe la zambarau, dogo na lenye kung’aa na laini.

Sina jiwe la zambarau bado, Marie aliwaza. Lingewekuwa zuri kwenye mkusanyiko wake.

Marie alitazama huku na kule. Bibi alikuwa kwenye meza nyingine. Hakuna mtu mwingine aliyekuwa karibu. Na hakuna yeyote atakayelikumbuka hili jiwe dogo, si ndiyo?

Marie akalichukua jiwe na kuliweka kwenye mfuko wake.

Usiku ule, akiwa na jiwe la zambarau kwenye sanduku lake la kidani, Marie aliingia kulala.

“Uko tayari kwa muda wa hadithi? Baba akaketi kitandani na kufungua gazeti la Rafiki .

Marie akajifunika blanketi lake na kusikiliza. Hadithi ilikuwa kuhusu mvulana ambaye alitubu baada ya kufanya uchaguzi mbaya.

Baba alipokuwa anasoma, Marie alihisi kama tumbo lilikuwa linasokota. Akajigeuza upande, kisha kugeuza foronya yake ya kulalia. Lakini hakuhisi vizuri. Na hakuacha kufikiria kuhusu lile jiwe la zambarau.

Picha
alt text

Baba alimaliza ile hadithi. “Je, uko SAWA?”

Marie hakujua cha kufanya. Kama akimwambia Baba, huenda angekasirika.

Lakini labda baba angejua jinsi ya kusaidia.

Polepole, Marie alijivuta kutoka kitandani na kutwaa lile jiwe la zambarau toka kwenye sanduku lake. “Nililichukua hili kutoka kwenye maktaba leo.” Machozi yalidondoka kutoka kwenye macho ya Marie. “Nisamehe sana.”

Baba alimpa kumbatio. “Daima ni SAWA kuniambia ukweli. Nina furaha juu yako kwa kuwa na ujasiri wa kuwa mwaminifu.”

Tumbo la Marie likaanza kuhisi vizuri. Baba hakukasirika!

“Na kwa sababu ya Yesu, sisi tunaweza kutubu. Kama vile katika hadithi hii,” baba alisema. Kwa nini tusilirejeshe jiwe kwenye maktaba?”

Marie alifumba macho yake kwa nguvu. “Hapana! Watakasirika.”

Baba aliweka mkono wake kwenye bega lake. “Wanaweza kukasirika kidogo. Lakini ninadhani watafurahia kwamba umelirudisha. Na itakufanya uhisi vizuri sana pia.”

Marie alivuta pumzi ndefu na kukubali kwa kichwa. “SAWA.”

Marie alitoa kipande cha karatasi na kuanza kuandika barua. “Samahani kwa kuchukua jiwe hili,” aliandika. “Natamani nisingekuwa nimefanya hivi kabisa. “Ninataka kufanya mambo kuwa sawa.”

Aliingiza ile barua kwenye bahasha. Kisha aliliweka lile jiwe dogo la zambarau ndani pia.

Picha
alt text

“Tutalirudisha kesho,” Baba alisema. “Je, unahisije sasa?”

“Vizuri,” Marie alisema. “Kuna kitu kimoja zaidi ninahitaji kufanya.”

Marie alipiga magoti kando ya kitanda chake na kusali. “Ninahisi vibaya kwa kutwaa jiwe hili,” alisema. “Kamwe sitaiba tena. Ninakushukuru Mungu kwa kunisaidia kuwa jasiri na mwaminifu.”

Alipokuwa anarudi kitandani, Marie alihisi amani. Kesho angeweza kurekebisha mambo yawe sawa. Na alijua Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wangemsaidia. Kwa sababu Yao, kila kitu kingekuwa SAWA.

Picha
PDF ya hadithi

Vielelezo na Katie Rewse