Hekalu ni nyumba ya Bwana. Hekalu hutuelekeza kwa Mwokozi wetu, Yesu Kristo. Katika mahekalu, tunashiriki katika ibada takatifu na kufanya maagano na Baba wa Mbinguni ambayo hutuunganisha kwake na kwa Mwokozi wetu. Maagano haya na ibada hizi zinatuandaa kurudi kwenye uwepo wa Baba wa Mbinguni na kuunganishwa pamoja kama familia milele.