2018
Sambaza Upendo wa Mungu
Oktoba 2018


Sambaza Upendo wa Mungu

Picha
Passing Along Gods Love

Mimi na familia yangu tulihamia Kentucky muda mfupi uliopita. Nilikuwa mwenye huzuni sana kwa sababu nilikuwa nawaacha marafiki zangu wote na jamaa zangu. Kentucky palikuwa ni pahali tofauti sana na kule nilikozoea. Kwa mara ya kwanza tulipoenda kanisani, niliona kwamba hakukuwa na watu wengi. Wakati nilipotambua ni kwa kiasi gani tawi langu lilikuwa dogo, niliamua kwamba badala ya kufikiria vibaya kulihusu, ningefanya kitu kulihusu.

Siku iliyofuata, mimi pamoja na mama yangu tulikwenda dukani. Kabla hatujaondoka nyumbani, nilichukua bunda la kadi. Tulipofika dukani, nilichukua peremende na kwenda kulipia. Keshia alipitisha peremende kwenye mashine, kisha akanipa. Nilimrudishia. Alionekana kuchanganyikiwa na akasema, “umekwisha ilipia, ma’am.”

Nikasema, “Najua, lakini ninakupa hii kama zawadi.” Kisha nikampa na kadi pamoja na peremende. Alitabasamu na kunishukuru. Aliangalia nyuma ya kadi, ambapo nilikuwa nimeandika “Kila mmoja ni mtoto wa Mungu.” Niliondoka nikiwa na furaha, nikijua kwamba hata kama hakujiunga na Kanisa, bado nilifanya kitu kizuri.

Baadae siku hiyo, nilikumbuka kwamba nilikuwa nimeacha kadi zilizobaki kwenye meza ya keshia! Wakati mwingine tulipoenda dukani, nilikwenda kuuliza kama bado zilikuwa pale. Kisha niliona kitu, nikasimama. Karibu meza tano za makeshia zilikuwa na kadi zilizosema “Kila mmoja ni mtoto wa Mungu.” Keshia alikuwa amezigawa. Nilihisi furaha kwa kile nilichokifanya.