Maandiko Matakatifu
2 Nefi 7


Mlango wa 7

Yakobo anaendelea kusoma kutoka katika Isaya: Isaya azungumza kimasiya—Masiya atakuwa na ulimi wa aliyeelimika—Atawapa mgongo Wake wale wampigao—Hatafadhaishwa—Linganisha Isaya 50. Karibia mwaka 559–545 K.K.

1 Ndiyo, kwani hivyo ndivyo asemavyo Bwana: Je, nimekuweka kando, au kukutenga milele? Na hivyo ndivyo asemavyo Bwana: Cheti cha talaka cha mama yako kiko wapi? Kwa nani nimekuweka, au ni kwa nani anayenidai nimekuuza? Ndiyo, kwa nani nimekuuza? Tazama, ni kwa uovu wenu ammejiuza, na ni kwa makosa yenu mama yenu ametengwa.

2 Kwa hivyo, nilipokuja, hakukuwepo mtu yeyote; anilipoita, ndiyo, hakukuwepo na yeyote wa kujibu. Ee nyumba ya Israeli, je, mkono wangu umefupishwa kwamba siwezi kukomboa, au sina uwezo wa kukomboa? Tazama, kwa kukemea kwangu ninakausha bbahari, ninafanya cmito yao kuwa nyika na dsamaki wao kunuka kwa sababu maji yao yamekauka, na wanakufa kwa sababu ya kiu.

3 Ninavisha mbingu na aweusi, na kusababisha bgunia iwe mavazi yao.

4 Bwana Mungu amenipatia aulimi wa aliyeelimika, kwamba niweze kujua jinsi ya kuwazungumzia katika majira, Ee nyumba ya Israeli. Wakati mmechoka anaamka asubuhi kwa asubuhi. Anaamsha sikio langu kusikia kama yule aliyeelimika.

5 Bwana Mungu amefungua asikio langu, na sikuasi wala kurudi nyuma.

6 Niliwapatia awalionipiga mgongo wangu, na mashavu yangu kwa waliongʼoa nywele. Sikuuficha uso wangu kutokana na aibu na kutemewa mate.

7 Kwani Bwana Mungu atanisaidia, kwa hivyo sitafadhaishwa. Kwa hivyo nimekaza uso wangu kama jiwe, na ninajua kwamba sitaaibishwa.

8 Na Bwana yuko karibu, na ananitetea. Nani atashindana na mimi? Tusimame pamoja. Nani adui yangu? Anikaribie mimi, na nitampiga kwa nguvu za kinywa changu.

9 Kwani Bwana Mungu atanisaidia. Na wale awatakaonihukumu, tazama, wote watakuwa wazee kama nguo, na kuliwa na nondo.

10 Ni nani miongoni mwenu anayemwogopa Bwana, anayetii asauti ya mtumishi wake, anayetembea kwa giza bila nuru?

11 Tazameni nyote mnaowasha moto, ambao mnajizingira kwa chembe za moto, tembeeni katika nuru ya moto awenu na kwa chembe za moto mnaowasha. Mtapata haya kutoka mkono wangu—mtalala chini kwa huzuni.