Misaada ya Kujifunza
TJS, Marko 16


TJS, Marko 16:3–6. Linganisha na Marko 16:4–7; Luka 24:2–4

Malaika wawili wanawasalimu wale wanawake kwenye kaburi la Mwokozi.

3 Lakini walipoangalia, waliona kuwa jiwe limeviringishwa mbali, (maana lilikuwa kubwa,) na malaika wawili wakiwa wamekaa juu yake, wakiwa wamevaa mavazi marefu meupe; nao wakaogopa.

4 Lakini wale malaika wakawaambia, Msiogope; ninyi mnamtafuta Yesu wa Nazareti; aliyesulubishwa; yeye amefufuka; hayupo hapa; angalieni mahali walipomlaza;

5 Nendeni zenu; mkawaambie wanafunzi wake na Petro, kwamba ametangulia Galilaya; huko mtamwona kama alivyowaambia.

6 Nao, walipoingia kaburini, walipaona mahali walipomlaza Yesu.