Mlango wa 25
Katika Ujio wa Pili, wenye kiburi na waovu watateketezwa kama makapi—Eliya atarejea kabla ya ile siku kubwa na ya kutisha—Linganisha Malaki 4. Karibia mwaka 34 B.K.
1 Kwani tazama, ile siku inakuja ambayo aitawaka kama tanuru; na wote wenye bkiburi, ndiyo, na wote wanaotenda maovu, watakuwa makapi; na ile siku inayokuja itawateketeza, asema Bwana wa Majeshi, kwamba haitawaachia shina wala tawi.
2 Lakini kwenu mnaolicha jina langu, yule aMwana wa Haki atawashukia na uponyaji katika mabawa yake; na ninyi mtaenda mbele na bkukua kama cndama zizini.
3 Na amtakanyaga waovu; kwani watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu katika siku nitakayofanya hivi, asema Bwana wa Majeshi.
4 Kumbukeni ninyi sheria ya Musa, mtumishi wangu, niliyemwamuru huko aHorebu kwa ajili ya Waisraeli wote, na amri za hukumu.
5 Tazama, nitawatumia aEliya nabii kabla ya kuja kwa ile bsiku kubwa na ya kutisha ya Bwana.
6 Na aatageuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, nisije na kupiga dunia na laana.