2020
Walikuwa na Tumaini la Kuja kwa Kristo—na Pia Sisi Tunaweza Kuwa Nalo
Aprili 2020


Walikuwa na Tumaini la Kuja kwa Kristo—na Pia Sisi Tunaweza Kuwa Nalo

Manabii katika Kitabu cha Mormoni walikuwa na tumaini kwamba Kristo angekuja. Kwa kusoma maneno yao, tunaweza kuwa na tumaini sawa na hilo kwa ajili ya wakati Atakapokuja tena.

Picha
Christ visiting the Americas

MATEMBEZI: Michoro na Jorge Cocco Santangelo

Ni maneno gani yanakujia akilini wakati unapofikiria kuhusu Kitabu cha Mormoni?

Wanefi, Walamani, -ites wa aina nyingine?

Vita, nyika, ole?

Toba, ukombozi, haki?

Yesu Kristo?

Tumaini?

Pasaka ni wakati mzuri zaidi wa kufikiria upya ujumbe wa Kitabu cha Mormoni. Muhimu zaidi, ujumbe kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwokozi na Mkombozi wetu. Kwa sababu Yake, tunaweza hatimaye kuwa huru kutoka kwenye uchungu wa mwili na nafsi. Kutoka kifo na dhambi. Tunaweza kushinda kila kitu kibaya ulimwengu unachotutupia.

Kwa urahisi, tunaweza kuwa na tumaini.

Tumaini—tumaini la kweli, linalolenga kwa Yesu Kristo—liliwatia msukumo manabii wa kale kuweka kumbukumbu kwenye bamba za dhahabu ambazo zingekuwa Kitabu cha Mormoni. Yakobo anatuambia “Kwani, kwa madhumuni haya tumeandika vitu hivi, ili wajue kwamba tulijua kuhusu Kristo, na tulikuwa na matumaini ya utukufu wake miaka mia mingi kabla ya kuja Kwake” (Yakobo 4:4; msisitizo umeongezwa).

Yakobo alitaka tujue kwamba yeye—na manabii wengine ambao waliweka kumbukumbu—walijua kuhusu kuja kwa Kristo. Mamia ya miaka kabla ya kuja Kwake! Na waliongozwa kuwa na tumaini hilo kutoka kwenye maneno ya manabii wao waliyosoma. Yakobo anaeleza, “na sio tu sisi pekee tuliokuwa na tumaini la utukufu Wake, lakini pia manabii wote watakatifu ambao walikuwa mbele yetu.

“Tazama, walimwamimi Kristo na kumwabudu Baba katika jina Lake, na pia sisi tunamwabudu Baba katika jina Lake. …

“Kwa hivyo, tunawachunguza manabii, na tunao ufunuo mwingi na roho ya unabii; pamoja na mashahidi hawa wote tunapokea tumaini, na imani yetu haiwezi kutingishwa” (Yakobo 4:4–6; ona pia 1 Nefi 19:21; Yakobo 7:11; Mosia 3:13; Helamani 8:16).

Tumaini ambalo walipata kutoka kwa yote mawili uzoefu wao wenyewe na unabii waliosoma katika maandiko uliwatayarisha kwa ajili ya siku ambayo Kristo angekuja. Vilevile, manabii leo hii wanatuhimiza tujitayarishe kwa ajili ya wakati Kristo atakaporudi tena. Ikiwa tunapaswa kuwa na tumaini sawa na hilo, sisi pia tunahitaji “kuwachunguza manabii, na [kutafuta] kuwa na ufunuo mwingi na roho ya unabii.” Ushuhuda wao wa Yesu Kristo hautaimarisha tu wetu lakini pia utatusaidia kujitayarisha kwa ajili ya ujio Wake.

Lehi

“Kwa hivyo, ni muhimu sana kuwajulisha wakazi wa dunia kuhusu vitu hivi, ili wajue hakuna binadamu anayeweza kuishi karibu na Mungu, bila fadhili, na rehema, na neema za Masiya Mtakatifu, ambaye anatoa maisha yake mwilini, na kuichukua tena kwa uwezo wa Roho, ili alete ufufuo wa wafu, akiwa wa kwanza kufufuka.”

Nefi

“Na tunazungumza kuhusu Kristo, tunafurahia katika Kristo, tunahubiri kuhusu Kristo, tunatoa unabii kumhusu Kristo, na tunaandika kulingana na unabii wetu, ili watoto wetu wajue asili ya kutegemea msamaha wa dhambi zao.”

Mfalme Benyamini.

“Na ataitwa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu. …

“Na lo, anawajia walio wake, ili wokovu uwafikie watoto wa watu hata kupitia imani kwa jina lake; … 

“Na atafufuka siku ya tatu kutoka kwa wafu. …

“Kwani tazama, na pia damu yake inalipiza dhambi za wale ambao wameanguka kwa sababu ya dhambi ya Adamu, ambao wameaga dunia bila kuelewa nia ya Mungu juu yao, au ambao wametenda dhambi bila kujua.”

Alma

“Na atakwenda, na kuteseka maumivu na masumbuko na majaribio ya kila aina; na hii kwamba neno litimizwe ambalo linasema atabeba maumivu na magonjwa ya watu wake.

“Na atajichukulia kifo, ili afungue kamba za kifo ambazo zinafunga watu wake; na atajichukulia unyonge wao, ili moyo wake ujae rehema, kulingana na mwili, ili ajue kulingana na mwili jinsi ya kuwasaidia watu wake kulingana na unyonge wao.”

Amuleki

“Na hivyo dhabihu kubwa na ya mwisho itakuwa Mwana wa Mungu, ndio, isiyo ya mwisho na milele.

“Na hivyo ataleta wokovu kwa wote ambao wataamini katika jina lake; hii ikiwa kusudi la hii dhabihu ya mwisho, kufungua tumbo la rehema, ambayo hupindua haki, na kuwafungulia wanadamu njia ya kupata imani na toba.

“Na hivyo rehema yaweza kutosheleza matakwa ya sheria, na kuwazungushia mikono ya usalama, wakati yeye ambaye hatumii imani hata kuweza kutubu anawekwa mbele ya sheria yote yenye kudai haki, kwa hiyo, yeye tu aliye na imani hata kuweza kutubu analetwa kwenye mpango ule mkuu na wa milele wa ukombozi.”

Picha
the Savior in Gethsemane

Gethsemane, by Jorge Cocco Santangelo

Samweli Mlamani

“Kwani tazama, lazima kwa kweli afe kwamba wokovu uje; ndio, inampasa yeye kwa lazima kwamba afe, ili kutimiza ufufuo wa wafu, kwamba kwa hiyo sababu binadamu waletwe kwenye uwepo wa Bwana.

“Ndio, tazama, hiki kifo huleta kutimiza ufufuo, na hukomboa binadamu wote kutokana na kifo cha kwanza—hicho kifo cha roho; kwani binadamu wote, kwa sababu ya kuanguka kwa Adamu wakitolewa kutoka uwepo wa Bwana, wanafikiriwa kama waliokufa, kwa vitu vya kimwili na vitu vya kiroho.

“Lakini tazama, ufufuko wa Kristo unakomboa binadamu, ndio, hata binadamu wote, na huwarejesha kwenye uwepo wa Bwana.”

Picha
Christ with children

Blessing the Children, by Jorge Cocco Santangelo

Mormoni

“Nataka mjue kwamba lazima muelimike kuhusu babu zenu, na mtubu dhambi zenu zote na maovu, na kuamini katika Yesu Kristo, kwamba yeye ni Mwana wa Mungu, na kwamba aliuawa na Wayahudi, na kwa uwezo wa Baba amefufuka tena, kwa kufanya hivyo amepata ushindi juu ya mauti; na pia kupitia kwake uchungu wa kifo umetolewa.

“Na anatimiza ufufuo wa wafu, ambako binadamu lazima atainuliwa kusimama mbele ya kiti cha hukumu.

“Na ameleta kutimizwa ukombozi wa ulimwengu, ambako yule ambaye atapatikana bila makosa mbele yake katika siku ya hukumu atakubaliwa kuishi kwenye uwepo wa Mungu katika ufalme wake, kuimba sifa zisizo na mwisho na jamii ya waimbaji wa juu, kwa Baba, na kwa Mwana, na kwa Roho Mtakatifu, ambao ni Mungu mmoja, katika hali ya furaha ambayo haina mwisho.”