2019
Kutokuwa Mwoga Kushiriki Ukweli
Oktoba 2019


Kutokuwa Mwoga Kushiriki Ukweli

Akiwa amejiami na ushuhuda wa injili pamoja na baraka za injili hiyo, Fabian hakuruhusu umri wake mdogo kumzuia kuwa mmisionari muumini mwenye nguvu, asiye na woga.

Picha
Fabian with missionaries

Jua linazama huko Las Tomas, ujirani uliojengwa juu ya mteremko wenye mchanga ukiangalia Antofagasta. Chini, mianga inaanza kung’ara pale siku inapomalizika katika jiji hili la bandari huko Chile ya kaskazini.

Ni Jumamosi usiku, na Fabian H. Mwenye miaka 13 angeweza kuwa akifurahia pamoja na rafiki zake. Lakini Fabian, muumini mpya wa Kanisa, badala yake anachagua kutumia jioni pamoja na wamisionari wa muda wote. Ni wakati wa “kusaidia kukusanya Israeli.”1

Kati ya waumini wote waliojitolea waliofanya kazi na Kellen VanNatter na Jordan Shelton wakati wa umisionari wao wa muda wote huko Chile, Fabian anang’aa kuliko wengine.

“Ikiwa alikuwa na muda, alikuwa nje pamoja na sisi tukifanya kazi ya umisionari,” anasema Kellen. “Wakati likizo ya majira ya joto ilipoisha, alikuwa na huzuni si kwa sababu alipaswa kurudi shule bali kwa sababu hakuwa na muda wa kutosha kwenda na sisi.”

Jordan, aliyekuwa mmisionari mwenza wa Kellen kwa miezi kadhaa, anaongeza, “Fabian yawezekana alikwenda pamoja nasi mara nne au tano katika wiki—kila wiki—wakati tulipotumikia pamoja Antofagasta. Alikuwa muumini mmisionari bora tuliyewahi kufanya naye kazi.”

Ni nini kinamfanya mvulana kuwa radhi kufanya kazi ya umisionari licha ya dharau kutoka kwa wanafunzi wenzake na kupuuzwa na watu asiowajua? Kwa Fabian, jibu liko katika baraka ambazo yeye na familia yake wamepata tangu walipoikubali injili—baraka anazotaka kushiriki na wengine.

Picha
Fabian teaching with missionaries

“Shangwe Isiyoelezeka”

Fabian alianza kujifunza masomo ya wamisionari muda mfupi baada ya wamisionari wa muda wote kuja na kugonga. Bado anakumbuka mkutano wake wa kwanza wa sakramenti.

“Sikumfahamu yeyote nilipoingia ndani ya jengo la ibada, hivyo nilikuwa kidogo mwoga,” anasema. “Lakini nilihisi kitu fulani cha ajabu. Nilihisi kama nilikuwa Kanisani kwa miezi au miaka.

Wakati wa ubatizo wake wiki chache baadaye, “nilihisi shangwe isiyoelezeka wakati wa kuzamishwa ndani ya maji na kuinuliwa juu tena. Nilihisi kama mtu mpya, nikijua kwamba nilikuwa ninakwenda kumfuata Yesu Kristo na kufanya kadiri niwezavyo kutii amri Zake.”

Pale wazazi wa Fabian ambao hawakuwa na ndoa, Leonardo na Angela, walipojiunga na kijana wao wakati wa masomo ya wamisionari, walijifunza kuhusu ndoa ya hekalu na familia za milele. “Wiki moja baadaye, baba yangu alipanga tarehe ya ndoa,” anasema Fabian. “Mama yangu alifurahi sana.”

Miezi minne baada ya Fabian kujiunga na Kanisa, Angela alimfuata kwenye maji ya ubatizo. “Hiyo ilikuwa ni baraka ya kupendeza,” anasema.

Baraka zingine haraka zilifuata. Leonardo, ambaye alikuwa amebatizwa akiwa mdogo, alirudi kwenye kushiriki kikamilifu Kanisani. Kujifunza injili kukawa jambo kuu nyumbani kwao. Wanafamilia wakakua pamoja. Leonardo alipata kazi ya kudumu. Na Fabian alipokea Ukuhani wa Haruni.

“Ninapenda kuwa na ukuhani ili kwamba niweze kupitisha sakramenti kwa waumini wa kata na kuwasaidia kufanya upya maagano yao,” anasema Fabian. “Nina furaha hasa wakati ninapopitisha kwa familia yangu na kwa wazee walionifundisha. Mtazamo wa kujivunia baba yangu anaonipa anaponiona nikipitisha sakramenti unanifanya niwe na furaha sana.”

Picha
Fabian with missionaries talking to a young man

“Hilo Lingekuwa la kupendeza Sana”

Fabian alianza kufanya kazi ya umisionari kabla hata hajabatizwa.

“Niliwaambia watatu kati ya rafiki zangu kwamba nitabatizwa. Wawili kati yao walikuja,” anasema. “Ninapenda kushiriki injili ili kwamba rafiki zangu waelewe kile tunachoamini na kile tunachofanya kanisani na ili kwamba waweze kujifunza injili, kubatizwa, na kuwa na maisha ya furaha. Ningekuwa na furaha ikiwa mmoja wao angebatizwa na kuwa mmoja wa washiriki wa akidi yangu. Hilo lingekuwa la kupendeza sana.”

Fabian anaenda shuleni na Kitabu cha Mormoni, na hubeba vipeperushi vya wamisionari kuwapa rafiki zake. Anafurahia kujibu maswali kuhusu Kanisa na kuwaalika marafiki kwenye mikutano ya Jumapili na usiku wa shughuli ya vijana. Na haogopi kuwaendea watu mtaani na, kama wamisionari walivyomfundisha, kuwaalika kujifunza kuhusu Kanisa na kujiandaa kwa ajili ya ubatizo.

“Fabian hajali ikiwa mtu anafikiria yeye ni wa ajabu kwa kushiriki ushuhuda wake,” anasema Kellen. “Anajua anafanya jambo sahihi. Anajua kwamba mambo ya kiroho ni muhimu kuliko kitu kingine chochote.”

Wakati Fabian anaposhiriki ushuhuda wake, Jordan anasema, anavuta nguvu kutoka kwenye uongofu wake, upendo wake wa injili, na baraka zake.

“Aliona baraka zilizokuja kwa familia yake, ndicho kitu kinachompa msukumo wa kuwa shujaa na mwenye kujiamini katika kushiriki injili na rafiki zake,” Jordan anasema. “Kuna wakati alikuwa akishuhudia kwa mchunguzi wa kanisa kuhusu vile ilivyokuwa baraka kwa wazazi wake kufunga ndoa lakini jinsi ilivyokuwa vigumu kwake kusubiri kwa miezi minne baada ya ubatizo wake kwa ajili ya mama yake kubatizwa. Hisia zake zilimzidi, na alitokwa machozi. Kisha alishuhudia kwamba ikiwa tutatii amri, Mungu atatupatia uangalizi.

Ushuhuda wa Fabian unamfanya kuwa muumini mmisionari mwenye nguvu, anaongeza Kellen.

“Yeye hayuko kama, ‘Ee, nilisikia mtu anasema hili kanisani.’ Badala yake, yeye daima hushiriki uzoefu wake mwenyewe binafsi—kama jinsi alivyohisi wakati alipokwenda kanisani kwa mara ya kwanza na jinsi anavyohisi anaposoma Kitabu cha Mormoni. Ni wa hakika na halisi.”

“Daima Ninajisikia Vizuri Zaidi”

Kwa Fabian, kushiriki injili huleta baraka nyingine.

“Wakati mwingine mambo mabaya hutokea shuleni, lakini kisha wamisionari huja kugonga mlangoni kwangu na kuuliza ikiwa ningekuwa tayari kuwasaidia kufundisha,” anasema. “Baada ya kwenda nao, ninahisi kana kwamba sina matatizo tena. Daima ninahisi vizuri zaidi wakati ninapokwenda nao, ninaposoma maandiko pamoja nao, na kuwasaidia kushiriki injili. Kushiriki injili na hadithi ya uongofu wangu huimarisha ushuhuda wangu. Na kufundisha injili kunanipa fursa ya kuwa mfano kwa wengine, ikijumuisha mdogo wangu wa kike.”

Haishangazi kwamba mojawapo ya lengo kubwa la Fabian ni kuwa mmisionari wa muda wote baada ya kuhitimu shule ya upili.

“Ninataka kushiriki ukweli pamoja na wale ambao hawaufahamu,” anasema. “Ninataka kuwaalika kuosha dhambi zao. Ninataka kuwafundisha jinsi wanavyoweza kuwa familia ya milele. Ninataka kuwaalika wawe na furaha sasa na kuishi katika hali ya furaha isiyo na mwisho baada ya maisha haya.”