2019
Je, Ninapaswa Kuendelea Kusoma?
Oktoba 2019


Je, Ninapaswa Kuendelea Kusoma?

Picha
Should I Keep Reading

Mwaka uliopita nilichukua kitabu katika maktaba kuhusu msichana ambaye alianzisha blogu. Nilidhani kingekuwa kitabu cha kufurahisha kwa sababu mhusika mkuu alikuwa na umri sawa na mimi, na mama yangu ni mwana blogu. Hivyo nilidhani kingekuwa kitabu ambacho ningeweza kujihusisha nacho.

Nilikuwa nimesoma kurasa chache tu za kitabu wakati msichana alipolitaja bure jina la Bwana. Sikupata hisia nzuri za ndani baada ya kusoma sehemu ile. Lakini niliendelea kusoma, nikitumaini lilikuwa jambo la mara moja tu. Nilisoma kurasa zingine kadhaa, na alilitaja tena.

Nilikwenda na kumwambia mama yangu kuhusu kile nilichopata. Sikujua ikiwa ninapaswa kuendelea kusoma au la. Mama yangu aliniambia uchaguzi ulikuwa wangu. Lakini alikubali pengine halikuwa jambo zuri kuendelea kusoma kama msichana alisema mambo ambayo tulijua ni mabaya. Mama yangu alisema kwamba haikuwa vizuri hasa kama msichana alikuwa akilitaja bure jina la Bwana.

Nilifikiria nitaona ikiwa lingetokea zaidi, hivyo nilisoma kitabu juujuu. Nilikuta kwamba kulitaja bure jina la Bwana ilikuwa ni jinsi msichana alivyokuwa akizungumza mara kwa mara. Niliamua kurudisha kitabu maktaba bila kukisoma zaidi.

Nilihisi huzuni kwamba mwandishi wa kitabu alilitaja bure jina la Bwana. Lakini baada ya kurudisha kitabu maktaba, nilihisi furaha kwamba nilifanya uchaguzi sahihi. Najua nilikuwa nikifuata “Viwango vyangu vya Injili kutoka kwenye kitabu changu cha Imani kwa Mungu ambacho kinasema, “Nitasoma na kutazama tu mambo ambayo yanampendeza Baba wa Mbinguni. Ninajua tunapaswa tu kutumia majina ya Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo kwa unyenyekevu na kwa heshima.