Misaada ya Kujifunza
TJS, Yohana 4


TJS, Yohana 4:1–4. Linganisha na Yohana 4:1–2

Mafarisayo wanatamani kumuua Yesu. Yeye anafanya baadhi ya ubatizo, lakini wanafunzi wake wanafanya zaidi.

1 Basi kwa hiyo Mafarisayo walipokuwa wamesikia kwamba Yesu alifanya na kuwabatiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana,

2 Walitafuta njia kwa bidii ili wapate kumwua; maana wengi walimkubali Yohana kama nabii, lakini hawakumwamini Yesu.

3 Sasa, Bwana alijua hili, ingawa yeye mwenyewe hakubatiza wengi kama walivyobatiza wanafunzi wake;

4 Maana yeye aliwaruhusu wao kuwa kama mfano wa namna wanavyopaswa kuonesha kuheshimiana, wakitangulizana.

TJS, Yohana 4:26. Linganisha na Yohana 4:24

Mungu anaahidii Roho Wake kwa waamini wa kweli.

26 Maana kwa hao Mungu ameahidi Roho wake. Nao wamwabuduo, imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.