Misaada ya Kujifunza
TJS, Waebrania 6


TJS, Waebrania 6:1–10. Linganisha na Waebrania 6:1–10

Kanuni za mafundisho ya Kristo hutupeleka katika ukamilifu.

1 Kwa hiyo, bila ya kuacha kanuni za mafundisho ya Kristo, na tuendelee hadi kuufikia ukamilifu; bila ya kujiwekea tena msingi wa toba itakanayo na matendo yaliyokufa, na wa imani kwa Mungu.

2 Na ya mafundisho ya ubatizo, ya kuwekea mikono, na ya ufufuo wa wafu, na ya hukumu ya milele.

3 Nasi tutaendelea kwenye ukamilifu kama Mungu anaruhusu.

4 Kwani ameifanya isiwezekane kwa wale ambao mwanzo walielimishwa, na wameonja karama za mbinguni, na walifanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5 Na wameonja neno jema la Mungu, na uwezo za ulimwengu ujao.

6 Kama watakengeuka, kurudishwa tena kupita toba; kwa kuwa walimsulubisha ndani yao Mwana wa Mungu upya, na kumwaibisha kwa wazi.

7 Kwani siku inakuja ambayo dunia inayokunywa wakati wa mvua inayonyesha mara kwa mara juu yake, na kutoa mimea kwa hao wanaoishi juu yake, na nani anayeivalisha, ambaye sasa anapokea baraka kutoka kwa Mungu, watasafishwa kwa moto.

8 Kwa kuwa kile kinachozaa miba na bingili kinakataliwa, na kikaribu kulaaniwa; kwahiyo kwa wale wanaozalisha matunda mabaya, watatupwa katika moto; kwani mwisho wao ni kuchomwa moto.

9 Lakini, wapendwa, tunashawishiwa na vitu vyenu vizuri, na vitu ambavyo vinaendana na wokovu, ingawa tunasema hivyo.

10 Kwani Mungu sio asiye na haki, kwa hiyo hatasahau kazi yako na kazi ya upendo, uliyoonesha kwa jina lake, katika hayo umewahudumia watakatifu, na unahudumia.