Mkutano Mkuu
Unaweza kuikusanya Israeli!
Mkutano mkuu wa Aprili 2021


Unaweza kuikusanya Israeli!

Nina hakika kabisa kwamba wewe kijana unaweza kufanya hili kwa sababu ya kitu kuhusu utambulisho wako na nguvu kubwa ndani yako.

Takribani miaka mitatu iliyopita, Rais Russell M. Nelson aliwaalika vijana wote wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho kujiandikisha katika “kikosi cha vijana cha Bwana ili kukusanya Israeli” pande zote mbili za pazia. Alisema, “Mkusanyiko huo ni jambo muhimu sana linalotokea duniani leo.”1 Nina hakika kabisa wewe kijana unaweza kufanya hili—na ukafanya vizuri sana—kwa sababu ya (1) kitu kuhusu utambulisho wako na (2) nguvu kubwa ndani yako.

Picha
Kaka na Dada Corbitt

Miaka arobaini na moja iliyopita, wamisionari wawili kutoka Kanisa letu walifika kwenye nyumba huko New Jersey, Marekani. Baada ya muda, kimiujiza, wazazi wote wawili na watoto wote 10 walibatizwa. Kwa maneno ya nabii, wao “waliacha Mungu ashinde”2 katika maisha yao. Ninapaswa kusema “maisha yetu.” Nilikuwa mtoto wa tatu. Nilikuwa na umri wa miaka 17 nilipoamua kufanya agano la kudumu la kumfuata Yesu Kristo. Je, unaweza kubashiri kingine nilichoamua? Nisingeweza kutumikia misheni. Hilo lilikuwa jambo kubwa mno. Na hii haingeweza kutarajiwa kutoka kwangu, sivyo? Nilikuwa mshiriki mpya kabisa wa Kanisa. Sikuwa na pesa Mbali na hilo, ingawa nilikuwa ndio nimehitimu kutoka shule ngumu zaidi ya upili huko Philadelphia Magharibi na nikakabiliwa na changamoto kadhaa za kutisha, niliogopa kuondoka nyumbani kwa miaka miwili mfululizo.

Picha
Familia ya Corbitt

Utambulisho Wako wa Kweli

Lakini ndio nilikuwa nimejifunza kwamba mimi na wanadamu wote tuliishi na Baba yetu wa Mbinguni kama wana na binti zake wa kiroho kabla ya kuzaliwa kwetu. Wengine walihitaji kujua, kama nilivyojua, kwamba Baba wa Mbinguni alitamani watoto Wake wote wafurahie maisha ya milele pamoja Naye. Kwa hivyo, kabla ya mtu yeyote kuwapo hapa duniani, aliwawasilisha wote na mpango wake kamili wa wokovu na furaha, pamoja na Yesu Kristo kama Mwokozi wetu. Kwa kusikitisha, Shetani alipinga mpango wa Mungu.3 Kulingana na kitabu cha Ufunuo, “kulikuwa na vita mbinguni”!4 Shetani kwa ujanja alidanganya sehemu ya tatu ya watoto wa kiroho wa Baba wa Mbinguni ili wamuache yeye ashinde badala ya Mungu.5 Lakini sio wewe! Mtume Yohana aliona kwamba ulimshinda Shetani “kwa neno la ushuhuda [wako].”6

Kujua utambulisho wangu halisi, nikisaidiwa na baraka yangu ya patriaki, ilinipa ujasiri na imani kukubali mwaliko wa Rais Spencer W. Kimball kukusanya Israeli.7 Vivyo hivyo itakuwa na kwenu, marafiki wapendwa. Kujua ulimshinda Shetani kwa neno la ushuhuda wako zamani kutakusaidia “kupenda, kushiriki, na kualika”8 sasa na siku zote—kuwaalika wengine waje na kuona, kuja na kusaidia, na kuja na kuwa sehemu ya, kama vita ile ile kwa ajili ya nafsi za watoto wa Mungu inaendelea.

Picha
Mzee Corbitt

Imani yenye Nguvu ndani Yako

Vipi kuhusu nguvu kubwa iliyoko ndani yako? Fikiria kuhusu hili: ulipiga kelele kwa furaha9 kuja katika ulimwengu ulioanguka ambapo wote wangekabiliwa na kifo cha mwili na kiroho. Hatungeweza kushinda sisi wenyewe. Hatungeteseka tu kutokana na dhambi zetu wenyewe lakini dhambi za wengine pia. Ubinadamu ungepitia karibu kila aina ya kuvunjika kunakofikirika na kukatishwa tamaa10—sote tukiwa na pazia la usahaulifu juu ya akili zetu na adui mbaya zaidi ulimwenguni akiendelea kutuwinda na kutujaribu. Matumaini yote ya kurudi tukiwa tumefufuliwa na safi kwenye uwepo mtakatifu wa Mungu yalitegemea kabisa kwa Mtu mmoja kutimiza ahadi Yake.11

Ni nini kilikupa nguvu ya kusonga mbele? Rais Henry B. Eyring alifundisha, “Ilihitaji imani katika Yesu Kristo kuuidhinisha mpango wa furaha na mahali pa Yesu Kristo katika mpango huo wakati wewe ulijua kidogo tu juu ya changamoto ambazo ungekumbana nazo katika maisha ya kufa.”12 Wakati Yesu Kristo alipoahidi kwamba Atakuja katika mwili na kutoa maisha yake ili kukukusanya13 na kukuokoa, kiujumla hukumwamini tu. Enyi “roho nzuri”14 mlikuwa na “imani kubwa mno” hata mkaona kwamba ahadi yake ni ya hakika.15 Hangeweza kudanganya, kwa hivyo ulimwona Yeye kama alikuwa tayari amemwaga damu yake kwa ajili yako, muda mrefu kabla ya kuzaliwa Kwake.16

Katika maneno ya mfano ya Yohana, “ulimshinda [Shetani] kwa damu ya Mwanakondoo.”17 Rais Dallin H. Oaks alifundisha kwamba katika ulimwengu huo “[mliona] mwisho tangu mwanzo.”18

Fikiria kwamba siku moja kabla ya kwenda shuleni, mmoja wa wazazi wako akatoa ahadi ya kweli kwamba unaweza kupata chakula chako pendwa utakaporudi nyumbani! Unafurahia! Wakati ukiwa shuleni unawaza kula chakula hicho, na unaweza hata kukionja. Bila kutarajia, unashiriki habari yako njema na wengine. Matarajio ya kurudi nyumbani yanakufurahisha sana kiasi kwamba mitihani na changamoto za shule huonekana myepesi. Hakuna kitu kinachoweza kuondoa furaha yako au kukufanya uwe na shaka kwa sababu ya uhakika wa ahadi hiyo! Vivyo hivyo, kabla ya nyie roho nzuri kuzaliwa, mlijifunza kuona ahadi za Kristo kwa njia hii ya uhakika, na mkaonja wokovu Wake.19 Imani yako kuu ni kama misuli ambayo hukua zaidi na zaidi kadiri unavyofanya mazoezi, lakini tayari misuli iko ndani yako.

Unawezaje kuamsha imani yako kubwa katika Kristo na kuitumia kukusanya Israeli sasa na kumshinda Shetani tena? Kwa kujifunza tena kutazama mbele na kuona kwa uhakika ule ule ahadi ya Bwana ya kukusanya na kuokoa leo. Kimsingi anatumia Kitabu cha Mormoni na manabii Wake kutufundisha jinsi inavyokuwa. Muda mrefu kabla ya Kristo, “manabii, na … makuhani, na … waalimu… [waliwashawishi watu] kumtazamia Masihi, na kumwamini kuja kwake kana kwamba tayari alikuwa.”20 Nabii Abinadi alifundisha, “sasa kama Kristo hangekuja ulimwenguni, akizungumza kuhusu vitu vitakavyokuja kama tayari vimeshakuja, hakungekuwa na ukombozi.”21 Kama Alma, Abinadi “alitazama mbele na jicho la imani”22 na kuona ahadi ya kweli ya Mungu ya wokovu ikiwa kama imekwishatimia tayari. “Walimshinda Shetani kwa damu ya Mwanakondoo na … neno la ushuhuda wao” muda mrefu kabla Kristo hajazaliwa, kama wewe ulivyofanya. Na Bwana aliwapa nguvu ya kualika na kukusanya Israeli. Atakufanyia vivyo hivyo unapotazamia mbele kwa imani, ukiona Israeli ikikusanywa—ulimwenguni kote na katika “sehemu zenu”23—na kuwaalika wote!

Mamia ya wamisionari walijenga juu ya imani yao katika Kristo yenye nguvu ya kabla ya kuzaliwa hapa duniani kwa kuwafikiria wale walioongea nao au kuwafundisha wakiwa wamevalia mavazi ya ubatizo na ya hekaluni. Katika hotuba yenye kichwa “Anza na Mwisho Akilini,”24 Rais Nelson alishiriki mfano wa kibinafsi wa kufanya hivi na aliwaamuru viongozi wa misheni kuwafundisha wamisionari wetu kufanya vivyo hivyo. Kwa kujua kwamba walitumia imani hii kuu katika Yesu Kristo kabla ya hapa duniani iliwasaidia sana wamisionari wetu wapendwa “kumsikiliza Yeye”25 na kuhuisha imani yao kubwa ya kukusanya Israeli kama Bwana alivyoahidi.

Kwa kweli, kudhani uwongo hudhuru imani.26 Rafiki zangu, kuwaza kwa makusudi au kutazama vitu ambavyo vinapingana na utambulisho wako, haswa ponografia, vitadhoofisha imani yako kwa Kristo na bila toba, zinaweza kuiharibu imani. Tafadhali tumia mawazo yako kuongeza imani katika Kristo, sio kuiharibu.

Programu ya Watoto na Vijana

Programu ya Watoto na Vijana ni zana ya kinabii ili kukusaidia wewe kijana kuimarisha imani yako kubwa. Rais Oaks alifundisha, “Programu hiyo imeundwa kukusaidia kuwa kama Mwokozi wetu katika maeneo manne: kiroho, kijamii, kimwili, na kiakili.”27 Ikiwa nyie vijana —mtaongoza— katika kuishi injili, kuwajali wengine, kuwaalika wote kupokea injili, kuunganisha familia milele, na kuandaa shughuli za kufurahisha,28 imani kubwa katika Kristo mliyokuwa nayo kabla ya maisha haya itaweka msingi na kuwapa nguvu ya kufanya kazi ya Bwana katika maisha haya!

Pia, malengo ya kibinafsi, “haswa malengo ya muda mfupi,”29 hukusaidia kurudisha imani yako yenye nguvu. Unapoweka lengo zuri, unatazamia mbele, kama ulivyofanya hapo awali, na kuona kile Baba yako wa Mbinguni anataka wewe au mtu mwingine kuwa.30 Kisha unapanga na kuweka bidii kulifikia lengo hilo. Mzee Quentin L. Cook alifundisha, “Kamwe usidharau umuhimu wa kupanga, kuweka malengo … na [kuwakaribisha wengine] —wote kwa jicho la imani.”31

Chaguo ni lako! Bwana alisema kuhusu nyie kwamba, “Nguvu [ya kuchagua] iko ndani yao.”32 Mzee Neil L. Andersen alielezea, “Imani yako itakua siyo kwa bahati nasibu, bali kwa kuchagua kwako.”33 Aliongeza, “maswali [yoyote] ya uaminifu [unayoweza kuwa nayo] … yatatatuliwa kwa uvumilivu na jicho la imani.”34

Nashuhudia kwamba (1) utambulisho wako wa kweli na (2) nguvu kubwa ya imani katika Kristo ndani yako itakuwezesha “kusaidia kuandaa ulimwengu kwa kurudi kwa Mwokozi kwa kuwaalika wote kuja kwa Kristo na kupokea baraka za Upatanisho Wake.”35 Naomba sote tushiriki furaha ya ahadi ya uhakika ya Kitabu cha Mormoni:

“Wenye haki wanaosikiza maneno ya manabii, na … kumtazamia Kristo kwa uthabiti … bila kujali mateso yote … hawataangamia.

“Lakini [Kristo] … atawaponya, na watakuwa na amani naye”36

Katika Jina la Yesu Kristo, amina.