Liahona
Tunazungumza kumhusu Kristo
Machi 2024


“Tunazungumza Kumhusu Kristo,” Liahona, Machi 2024.

Kwa ajili ya Wazazi

Tunazungumza Kumhusu Kristo

Picha
mama na watoto wakiwa wamekaa mezani

Mstari wa hisani

Wapendwa Wazazi,

Nefi aliwafundisha watu wake jinsi ilivyo muhimu kumweka Bwana katika sehemu ya mbele kabisa ya maisha yetu. Aliandika, “Tunazungumza kumhusu Kristo, tunafurahia katika Kristo, tunahubiri kuhusu Kristo, tunatoa unabii kumhusu Kristo, na tunaandika kulingana na unabii wetu, ili watoto wetu wajue asili ya kutegemea msamaha wa dhambi zao” (2 Nefi 25:26). Ungeweza kurejea upya mada zifuatazo pamoja na familia yako na watu wengine unaowapenda ili kuwaonesha kwenye injili ya Yesu Kristo, kwenye mwongozo Wake, na kwenye kanuni za hekima ambazo zitatusaidia tumtafute Yeye katika ulimwengu wa kisasa, wenye shughuli nyingi.

Mijadala ya Injili

Injili ya Yesu Kristo ni kwa ajili ya Kila Mmoja

Watu wote wanahitaji tumaini na ukombozi unaotolewa na injili na Upatanisho wa Yesu Kristo. Jadiliana na familia yako baadhi ya mafundisho kutoka kwenye makala ya Mzee Jeffrey R. Holland juu ya jinsi unavyoweza kupenda, kushiriki, na kumwalika mtu fulani aipokee na kuikumbatia injili ya Yesu Kristo (ona ukurasa wa nne).

Kanuni za Hekima kwa ajili ya Matumizi ya Vyombo vya Habari

Teknolojia na vyombo vya habari ni vifaa vyenye msaada wakati vinapotumika kwa usahihi. Rejelea baadhi ya kanuni kwenye ukurasa wa 22 na jadili viwango vya familia yako kwenye matumizi ya vyombo vya habari. Kwa kutumia “maswali ya kutafakari,” fikiria kile kinachokwenda vyema na nini kingeweza kuboreshwa.

Kumfuata Mwokozi katika Imani

Katika makala hii kwenye ukurasa wa 40, Mzee Benjamin M. Z. Tai anashiriki njia nne ambazo kwazo Mwokozi anatusaidia sisi. Baada ya kurejea upya njia hizi pamoja na familia yako, jadili jinsi ulivyosaidiwa kadiri ulivyomfuata Mwokozi katika Imani.