Agano la Kale 2022
Machi 21–27. Kutoka 1–6: “Nimekumbuka Agano Langu”


“Machi 21–27. Kutoka 1–6: ‘Nimekumbuka Agano Langu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Machi 21-27. Kutoka 1–6,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
Musa na Kichaka Kinachowaka moto

Musa na Kichaka Kinachowaka Moto, na Harry Anderson

Machi 21–27

Kutoka 1–6

“Nimekumbuka Agano Langu”

Anza kujifunza kwa maombi, na omba kwa ajili ya msaada wa kupata ujumbe katika Kutoka 1–6 ambao unahusu maisha yako na kwa huduma yako katika ufalme wa Mungu.

Andika Misukumo Yako

Mwaliko wa kuishi Misri kwa kweli uliokoa familia ya Yakobo. Lakini baada ya mamia ya miaka, wazao wao walifanywa watumwa na kufanyiwa ukatili na farao mpya “ambaye hakumjua Yusufu” (Kutoka 1:8). Ingekuwa kawaida kwa Waisraeli kujiuliza kwa nini Mungu ameruhusu hili litokee kwao, watu Wake wa agano. Je, alilikumbuka agano alilofanya nao? Bado wao walikuwa watu Wake? Je aliweza kuona ni kiasi gani walikuwa wakiteseka?

Yawezekana kuna wakati umejisikia kujiuliza maswali kama haya. Yawezekana ukajiuliza, Je, Mungu anajua hiki ninachopitia? Je, anaweza kusikia kilio changu kwa ajili ya msaada Hadithi ya ukombozi wa Israeli kutoka Misri katika kitabu cha Kutoka inajibu maswali ya aina hiyo kwa uwazi kabisa: Mungu hasahau watu Wake. Anakumbuka maagano yake na sisi na atayatimiza katika wakati Wake mwenyewe na katika njia yake (ona Mafundisho na Maagano 88:68). “Nitawakomboeni kwa mkono ulionyooshwa,” Yeye anatamka. “Mimi ni Bwana Mungu wenu, niwatoaye ninyi kutoka chini ya mizigo [yenu]” (Kutoka 6:6–7).

Kwa ajili ya muhtasari wa kitabu cha Kutoka, ona “kitabu cha Kutoka” katika Kamusi ya Biblia.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Kutoka 1–2

Yesu Kristo ni Mkombozi wangu.

Moja ya dhima kuu katika kitabu cha Kutoka ni kwamba Mungu ana uwezo wa kuwaweka huru watu Wake kutokana na ukandamizaji. Kutawaliwa kiutumwa kwa Waisraeli kama ilivyoelezewa katika Kutoka 1 kunaweza kuonekana kama ishara ya kuwa kifungoni kitu ambacho sisi sote tunakabiliwa nacho kwa sababu ya dhambi na mauti (ona 2 Nefi 2:26–27; 9:10; Alma 36:28). Na Musa, mkombozi wa Waisraeli, anaweza kuonekana leo kama mfano, au mwakilishi, wa Yesu Kristo (ona Kumbukumbu la Torati 18:18–19; 1 Nefi 22:20–21). Soma Kutoka 1–2 ukiwa na milingano hii akilini. Unaweza kutambua, kwa mfano, kwamba wote Musa na Yesu Kristo waliokolewa kutokana na mauti wakiwa watoto wadogo (ona Kutoka 1:222:10; Mathayo 2:13–16) na kwamba wote walikaa nyikani kabla ya kuanza huduma zao (ona Kutoka 2:15–22; Mathayo 4:1–2). Je, ni utambuzi gani mwingine unajifunza kutoka katika kitabu cha Kutoka kuhusu kifungo cha kiroho? Kuhusu ukombozi wa Mwokozi?

Ona pia D. Todd Christofferson, “Ukombozi,” Liahona, Mei 2013, 109–12.

Picha
Mtoto Musa akiwa katika jamanda

Moses in the Bulrushes, © Providence Collection/licensed kutoka goodsalt.com

Kutoka 3–4

Mungu anatoa uwezo kwa wale anaowaita kutenda kazi Yake.

Leo tunamjua Musa kama nabii mkuu na kiongozi. Lakini Musa mwenyewe hakujiona hivyo wakati Bwana mara ya kwanza alipomwita. “Mimi ni nani,” Musa alijiuliza, “kwamba napaswa kwenda kwa Farao?” (Kutoka 3:11). Bwana, hata hivyo, alijua Musa hasa ni nani—na angeliweza kuwa nani. Unaposoma Kutoka 3–4, angalia jinsi Bwana alivyomhakikishia Musa na alivyojibu mashaka yake. Je, unapata nini katika milango hii ambacho kinaweza kukupa mwongozo wa kiungu wakati unapojiona kuwa una mapungufu? Je, ni kwa jinsi gani Bwana anawabariki watumishi Wake kwa ongezeko na uwezo wa kufanya mapenzi Yake? (ona Musa 1:1–10, 24–39; 6:31–39, 47). Je, ni wakati gani umeona Mungu akifanya kazi Yake kupitia wewe au wengine?

Kwa nyongeza kuhusu maisha na huduma ya Musa, ona “Musa” katika Kamusi ya Biblia au Mwongozo wa Maandiko.

Kutoka 5-6

Madhumuni ya Bwana yatatimizwa katika wakati Wake mwenyewe.

Ingawa Musa kwa ujasiri alienda mbele ya Farao, kama Bwana alivyomwamuru, na kumwambia awaachilie Waisraeli, Farao alikataa. Ukweli ni kwamba, yeye alifanya maisha ya Waisraeli kuwa magumu zaidi. Musa na Waisraeli wangeweza kujiuliza kwa nini mambo yalikuwa hayaendi hata wakati ambapo Musa alikuwa akifanya kile Mungu alichomwambia afanye (ona Kutoka 5:22–23).

Je, umewahi kujisikia kuwa ulikuwa ukifanya mapenzi ya Mungu lakini hukuyaona mafanikio uliyokuwa ukitarajia? Rejelea Kutoka 6:1–8, ukitafuta kitu ambacho Bwana alisema ili kumsaidia Musa kuvumilia. Je, ni kwa jinsi gani Bwana amekusaidia wewe kuvumilia katika kufanya mapenzi Yake?

Kutoka 6:3

Je, Yehova ni nani?”

Yehova ni moja ya majina ya Yesu Kristo na linatupeleka kwa Mwokozi kabla hajazaliwa. Tafsiri ya Joseph Smith inafafanua kwamba manabii Ibrahimu, Isaka na Yakobo walimjua Bwana kwa jina hili (ona Kutoka 6:3, tanbihi c). Kwa kawaida, wakati kifungu cha maneno “Bwana” kinapoonekana katika Agano la Kale, kinatupeleka kwa Yehova. Katika Kutoka 3:13–15, jina “MIMI NIKO” pia ni jina la Yehova (ona pia Maafundisho na Maagano 38:1; 39:1).

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Kutoka 1:-2.Wanawake wengi walifanya kazi muhimu sana katika mpango wa Mungu wa kumwinua mkombozi kwa ajili ya Waisraeli. Kama familia, mngeweza kusoma kuhusu wakunga Shifra na Pua (Kutoka 1:15–20); Mama wa Musa, Yokabedi, na dada yake, Miriamu (Kutoka 2:2–9; Hesabu 26:59); binti wa Farao (Kutoka 2:5–6, 10); na Sipora mke wa Musa (Kutoka 2:16–21). Je, ni kwa jinsi gani wanawake hawa waliendeleza mpango wa Mungu? Je, ni kwa jinsi gani matukio yao yanatukumbusha juu ya misheni ya Yesu Kristo? Unaweza pia kukusanya picha za ndugu zako wanawake na wahenga na simulia hadithi zao. Je, ni kwa namna gani sisi tumebarikiwa kwa sababu ya wanawake waaminifu? Ujumbe wa Rais Russell M. Nelson “Ombi kwa Dadaa Zangu” (Liahona, Nov. 2015, 95–98) unaweza kuongezea kwenye majadiliano yenu.

Kutoka 3:1–6.Wakati Musa alipokiendea kichaka kinachowaka moto, Bwana alimwambia avue viatu vyake kama ishara ya heshima kuu. Tunawezaje kuonyesha heshima kwa ajili ya mahali patakatifu? Kwa mfano, tunaweza kufanya nini ili kufanya nyumba zetu kuwa mahali patakatifu ambapo Roho wa Bwana anaweza kukaa? Je, tunawezaje kuonyesha heshima kuu zaidi katika sehemu nyingine takatifu?

Kutoka 4:1–9.Bwana alimpatia Musa nguvu ya kufanya miujiza mitatu kama alama ya kuonyesha wana wa Israeli kwamba Yeye alikuwa amemtuma Musa. Je, alama hizi zinatufundisha nini kuhusu Yesu Kristo?

Kutoka 5:2.Je ingeweza kumaanisha nini kwa sisi “kumjua” Bwana? Je, ni kwa jinsi gani tunakuja kumjua Yeye? (Kwa mfano, ona Alma 22:15–18). Je, ni kwa jinsi gani uhusiano wetu sisi na Yeye unavyogusa hamu yetu ya kumtii Yeye? (Ona pia Yohana 17:3; Mosia 5:13).

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Reverence Is Love,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto,31.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tunza shajara ya kujifunzia. Unaweza kuona kuwa inasaidia kutumia shajara au daftari kuandika mawazo, dhana, maswali au taswira zinazokujia wakati unaposoma.

Picha
Binti wa Farao anamwona mtoto Musa

Musa Anaokotwa katika Manyasi na Binti wa Farao, na George Soper