Katika kipindi chote hiki, washiriki wa Urais wa Kwanza na Akidi ya Mitume Kumi na Wawili wamezungumza mara kwa mara kuhusu ibada na maagano ya hekaluni. Hapa chini ni nukuu kadhaa, zilizoandaliwa kwa mada, ambazo zinaonyesha jinsi mada hizi takatifu zilivyojadiliwa katika mipangilio tofauti. Bofya ili kukuza sehemu. Inapowezekana, kiungo hutolewa ili kufikia nyaraka halisi.
Ubatizo na Uthibitisho
Rais Russell M. Nelson
“Wakati wowote unapofanya kitu chochote kinachomsaidia mtu yeyote—upande wowote wa pazia—kuchukua hatua kuelekea kufanya maagano na Mungu na kupokea ibada zao muhimu za ubatizo na za hekaluni, unasaidia katika kukusanya Israeli. Ni rahisi tu kama hivyo.”
Hope of Israel, worldwide youth devotional, Juni 3, 2018
Rais Thomas S. Monson
“Na sasa, marafiki zangu wadogo mko kwenye miaka ya ujana, kila wakati, muwe na hekalu katika maono yenu. Usitende chochote kitakachokuzuia kuingia malango yake na kushiriki baraka takatifu na za milele huko. Ninawapongeza wale wenu ambao huenda hekaluni mara kwa mara kufanya ubatizo kwa niaba ya wafu, wakiamka masaa ya asubuhi sana ili kushiriki ubatizo kabla ya shule kuanza. Sidhani kuna njia bora zaidi ya kuianza siku zaidi ya hiyo.”
The Holy Temple—A Beacon to the World, April 2011 general conference
Mzee David A. Bednar
“Ninawaalika vijana wa Kanisa kujifunza kuhusu na kupata uzoefu wa Roho ya Eliya. Ninawahimiza kujifunza, kutafiti mababu zenu, na kujitayarisha kufanya ubatizo wa uwakilishi katika nyumba ya Bwana kwa jamaa zenu waliofariki [ona Mafundisho na Maagano 124:28–36]. Ninawahimiza kuwasaidia watu wengine kutambua historia za familia zao Mnapoitikia kwa imani mwaliko huu, mioyo yenu itawageukia mababu. … Ushuhuda wenu na kuongoka katika Mwokozi kutakuwa kwa kina na kwa kudumu. Nami ninawaahidi mtalindwa dhidi ya ushawishi uliopamba moto wa adui. Unaposhiriki katika kazi hii takatifu na kuipenda, utalindwa katika ujana wako na katika maisha yako.”
The Hearts of the Children Shall Turn, October 2011 general conference
Mzee Quentin L. Cook
“Mchanganyiko wa kuongezeka kwa idadi ya mahekalu na maendeleo ya kiteknolojia katika kutimiza majukumu yetu matakatifu ya historia ya familia ya mababu zetu inafanya wakati huu kuwa wenye baraka zaidi katika historia yote. Ninafurahia katika uaminifu wa ajabu wa vijana wetu katika kuorodhesha na kutafuta mababu zao na kisha kufanya kazi ya ubatizo na uthibitisho katika hekalu. Katika hali halisi ninyi ni miongoni mwa waokoaji waliotabiriwa kwenye Mlima Sayuni.”
Jione Mwenyewe Hekaluni, mkutano mkuu wa Aprili 2016
Mzee Gary E. Stevenson
“Urais wa Kwanza umewaalika ‘waumini watu wazima kuwa na kibali cha hekalu na kutembelea hekalu mara nyingi zaidi’ ambapo muda na hali inaruhusu na kuwaomba waumini ‘kutumia muda wa baadhi ya shughuli za burudani kwa huduma ya hekalu.’ Pia waliwahimiza ‘waumini wapya na vijana wa Kanisa ambao wana umri wa miaka 12 na zaidi kuishi kwa ustahiki ili kusaidia katika kazi hii kuu kwa kutumikia kama wawakilishikwenye ubatizo na uthibitisho.’ [Barua ya Urais wa Kwanza, Machi 11, 2003.]”
Sacred Homes, Sacred Temples, April 2009 general conference
Mzee Richard G. Scott
“Je, ninyi vijana wadogo mnataka kupunguza nguvu za adui katika maisha yenu? Jitoleeni katika kutafuta mababu zenu, tayarisha majina yao kwa ajili ya ibada takatifu za uwakilishi zinazopatikana hekaluni, na kisha nenda hekaluni kusimama kama mwakilishi wao kwa kupokea ibada ya ubatizo na kipawa cha Roho Mtakatifu. Kadiri unavyokuwa mkubwa, utaweza kushiriki katika kupokea ibada nyingine pia. Sidhani kama kuna ulinzi mkubwa zaidi kutokana na ushawishi wa adui katika maisha yako kuliko huu.”
The Joy of Redeeming the Dead, October 2012 general conference
Gamenti za Hekaluni na Nguo za Ibada
Rais Russell M. Nelson
“Kuvaa gamenti za hekaluni huwa na ishara muhimu ya kina. Huwakilisha dhamira endelevu. Kama vile Mwokozi alivyoonyesha mfano wa kuvumilia hadi mwisho, tunavaa gamenti kwa uaminifu kama sehemu ya vazi la ustahimilivu la Mungu. Hivyo ndivyo tunavyoonyesha imani yetu Kwake na katika maagano Yake ya milele pamoja nasi.”
Personal Preparation for Temple Blessings, April 2001 general conference
Rais Russell M. Nelson
“Ikiwa ungependa kujua zaidi kuhusu mambo ya kale ya mavazi ya hekaluni, tafuta mwenyewe katika Agano la Kale. Agano la Kale limejaa marejeo ya mavazi maalumu ya hekaluni.”
Teachings of Russell M. Nelson, 372
Rais Boyd K. Packer
“Kuhusiana na ibada hizi, katika hekalu utavikwa rasmi garmenti na kuahidiwa baraka za ajabu kuhusiana nayo. Ni muhimu kwamba usikilize kwa makini wakati ibada hizi zinapotolewa na kwamba unajaribu kukumbuka baraka zilizoahidiwa na masharti ambayo kwazo baraka hizi hutolewa.”
Nguo Takatifu za Hekaluni
“Majoho ya hekaluni ya Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, yanayojulikana kama majoho ya ukuhani mtakatifu, huvaliwa tu ndani ya mahekalu ya Watakatifu wa Siku za Mwisho na hubakia kwa ajili ya sakramenti za juu za imani. Weupe huashiria usafi. Hakuna alama wala cheo. Mtume mwandamizi na muumini mpya hawatofautiani wakiwa wamevaa kwa namna sawa. Wanaume na wanawake huvaa mavazi ya aina moja. Mavazi ya kawaida huunganisha ishara ya kidini yakiakisi mambo ya kale yaliyojidhihirisha katika maandiko ya kale kutoka kwenye kitabu cha Kutoka.”
Nguo Takatifu za Hekaluni
“Watakatifu wengi waaminifu wa Siku za Mwisho huvaa gamenti kama nguo ya ndani ambayo ina umuhimu mkubwa kidini. Ikiwa sawa kimtindo na nguo ya kawaida ya ndani, huwa limegawanyika sehemu mbili na kawaida hujulikana kama ‘gamenti ya hekaluni.’ … Gamenti ya hekaluni huvaliwa na waumini watu wazima wa Kanisa ambao wamefanya ahadi takatifu za uaminifu kwa amri za Mungu na injili ya Yesu Kristo katika mahekalu ya Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho. Kwa waumini wa Kanisa, gamenti ya hekaluni, iliyovaliwa kabla ya mavazi ya kawaida, pamoja na mavazi ya mfano yaliyovaliwa wakati wa ibada ya hekaluni, huwakilisha kipengele kitakatifu na cha kibinafsi cha uhusiano wao na Mungu na kujitolea kwao kuishi maisha mema, yenye heshima.”
Uanzishwaji wa Endaumineti - Kuosha na Kupakwa Mafuta
Rais Gordon B. Hinckley
“Kuna lengo baada ya Ufufuko. Lengo hilo ni kuinuliwa ili kuwepo kwenye ufalme wa Baba yetu. Hili litafanikiwa kupitia utii wa amri za Mungu. Huanza kwa kumkubali yeye kama Baba yetu wa Milele na mwanawe kama Mwokozi wetu aliye hai. Huusisha ushiriki katika ibada mbalimbali, kila moja ikiwa ni ya muhimu na ya kuhitajika. Ya kwanza katika hizo ni ubatizo kwa kuzamishwa katika maji, ambayo, kulingana na Mwokozi, bila hiyo, mtu hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu. Kisha lazima kufuatiwa na kuzaliwa kwa Roho, kipawa cha Roho Mtakatifu. Kisha katika mfululizo kwa miaka ijayo, kwa wanaume, kutawazwa kwenye ukuhani, ikifuatiwa na baraka za hekaluni kwa wote wanaume na wanawake ambao wanastahili kuingia ndani yake. Baraka hizi za hekaluni ni pamoja na kuoshwa na kupakwa mafuta ili tuwe safi mbele za Bwana. Hujumuisha huduma ya mafundisho ambayo tunapewa endaumenti ya majukumu na baraka ambazo zinatuhamasisha kuwa na tabia inayoendana na kanuni za injili. Hujumuisha ibada za kuunganisha ambapo kile kilichofungwa duniani kimefungwa mbinguni, zikitoa mwendelezo wa familia.”
Temples and Temple Work, Ensign, February 1982
Rais Spencer W. Kimball
“Joseph Smith aliwapa mitume kumi na wawili funguo zote na mamlaka na uwezo ambao yeye mwenyewe alikuwa nao na alivyokuwa amevipokea kutoka kwa Bwana. Aliwapa kila endaumenti, kila mwosho na upakwaji mafuta, na akawapa ibada za kuunganisha.”
We Thank Thee, O God, for a Prophet, October 1972 general conference
Rais Boyd K. Packer
“Ibada za kuoshwa na kupakwa mafuta hurejelewa mara nyingi hekaluni kama ibada za awali. Itakuwa vya kutosha kwa madhumuni yetu kwa kusema tu yafuatayo: Vinavyohusiana na endaumenti ni kuoshwa na kupakwa mafuta—kiuhalisia kwa ishara, lakini kuahidiwa baraka dhahiri, baraka za sasa na baraka zijazo.”
Preparing to Enter the Holy Temple
Mzee James E. Talmage
“Kaskazini mwa sehemu ya kubatizia kuna vyumba vipana na vizuri vya kubadilishia nguo vinavyotumiwa na akina kaka, na kusini ni vyumba sawa na hivyo vya akina dada. Vifaa pia huwekwa kwenye vyumba ambapo baadhi ya ibada za kupakwa mafuta hufanyika. Katika ibada hizi wanawake huwahudumia wanawake, na wanaume huwahudumia wanaume.”
The House of the Lord [1976], 83
Mzee Robert D. Hales
“Katika hekalu, mpango wa wokovu huelezwa na maagano matakatifu hufaywa. Maagano haya, pamoja na kuvaa gamenti takatifu za hekaluni, humuimarisha na kumlinda mtu aliyefanya endaumenti dhidi ya nguvu za adui. Baada ya kupokea endaumenti zao wenyewe, kijana au msichana anaweza kuhudhuria hekaluni na kufanya ibada za uwakilishi ili kutoa baraka za ukuhani kwa wale ambao wamefariki bila fursa ya kupokea baraka hizi wakati wa maisha ya duniani.”
Blessings of the Priesthood, October 1995 general conference
Maelezo ya Endaumenti
Rais Russell M. Nelson
“Hekalu kwa kweli limejaa ukweli. Kweli za mpango wa Baba zimewekwa wazi kwetu kwa uwazi na nguvu. Maneno ya kweli kuhusu Baba yetu, Mwana Wake, na Uhusiano Wao kwetu yameongelewa katika maagano na ibada za hekaluni. Hekalu ni nyumba ya ufunuo ambapo ukweli unaenea juu ya nafsi zetu na kuangaza ufahamu wetu [ona Mafundisho na Maagano 109:15]. Tunajifunza kuhusu utambulisho wetu wa milele na kusudi na ahadi za ajabu za Bwana. Ahadi hizo ni za kweli, kwa maana Mungu wetu ni Mungu wa kweli na hawezi kusema uongo [ona Etheri 3:2]. … Ikiwa kaka na dada zetu wanakwenda hekaluni wakitafuta nguvu na ufahamu, watafundishwa na Bwana Mwenyewe kuhusu kweli ambazo ni muhimu sana kwao wakati wa shida.”
Teachings of Russell M. Nelson, 373
Rais Ezra Taft Benson
“Sheria za selestia, zilizojumuishwa katika ibada fulani za Kanisa la Yesu Kristo, zinafuatwa kwa maagano ya hiari. Sheria ni za kiroho. Hivyo, Baba yetu wa Mbinguni ametawaza baadhi ya sehemu takatifu, ziitwazo mahekalu, ambamo sheria hizi zinaweza kuelezewa kikamilifu. Sheria zinajumuisha sheria ya utiifu na ya dhabihu, sheria ya injili, sheria ya usafi wa kimwili na sheria ya kuweka wakfu.”
A Vision and a Hope for the Youth of Zion, Brigham Young University devotional, Aprili 12, 1977
Rais Boyd K. Packer
“Huko waumini wa Kanisa ambao wanajiweka wastahiki wanaweza kushiriki katika ibada takatifu zaidi na za kuinuliwa za ukombozi ambazo zimefunuliwa kwa mwanadamu. Huko tunaweza kuoshwa na kupakwa mafuta na kuagizwa na kufanyiwa endaumenti na kufunganishwa. Na wakati tunapokuwa tumepokea baraka hizi kwa ajili yetu wenyewe, tunaweza kufanya kwa niaba ya wale ambao wamefariki bila kupata fursa sawa na hiyo.”
Come to the Temple, Ensign, October 2007
Mzee Robert D. Hales
“Matamanio yetu ya kurudi kwa Baba wa Mbinguni huongezeka kama sisi, kwa kuongezea kwenye kuchukua sakramenti, tutastahili kupata kibali cha hekaluni. … Kisha, kama watu waliofanyiwa endaumenti hekaluni, tunaanzisha mifumo ya kuishi kama Kristo. Hii ni pamoja na utii, kutoa dhabihu ili kushika amri, kupendana, kuwa na adabu katika mawazo na matendo na kujitoa wenyewe kujenga ufalme wa Mungu. Kupitia Upatanisho wa Mwokozi na kwa kufuata mifumo hii ya msingi ya uaminifu, tunapokea ‘nguvu kutoka juu’ ili kukabiliana na changamoto za maisha. Tunahitaji zaidi nguvu hii ya kiungu leo kuliko hapo awali. Ni nguvu tunayopokea tu kupitia ibada za hekaluni.”
Coming to Ourselves: The Sacrament, the Temple, and Sacrifice in Service, April 2012 general conference
Mzee James E. Talmage
“Endaumenti ya hekalu, kama inavyotolewa katika mahekalu ya kisasa, inajumuisha maagizo yanayohusiana na umuhimu na mlolongo wa vipindi vya zamani. … Wakati huu wa mafundisho inajumuisha kumbukumbu ya matukio maarufu zaidi ya kipindi cha uumbaji, hali ya wazazi wetu wa kwanza katika Bustani ya Edeni, kutotii kwao na hatimaye kufukuzwa kutoka kwenye makao hayo yenye furaha, hali yao katika ulimwengu wa upweke na unaochosha baada ya kuamriwa kuishi kwa kazi na jasho, mpango wa ukombozi ambao uvunjaji mkubwa wa sheria unaweza kulipiwa.”
The House of the Lord [1976], 84
Mzee James E. Talmage
“Ibada za endaumenti zinajumuisha majukumu fulani kwa upande wa mtu binafsi, kama vile agano na ahadi ya kutii sheria ya wema na usafi wa kimwili, kuwa na hisani, ukarimu, uvumilivu na usafi; kujitolea talanta na nyenzo kwa kueneza ukweli na kuinua jamii [ya binadamu]; kudumisha ibada kwa ajili ya ukweli; na kutafuta kwa kila njia kuchangia katika maandalizi makuu ili dunia iweze kuwa tayari kumpokea Mfalme wake—Bwana Yesu Kristo. Kwa kuchukua kila agano na kuchukua kila wajibu baraka iliyoahidiwa inatamkwa, kulingana na utunzaji wa uaminifu wa masharti.”
The House of the Lord, 100
Sheria ya Utiifu
Rais Thomas S. Monson
“Kaka na dada zangu, jaribio kuu la maisha haya ni juu ya utiifu. ‘Nasi tutawajaribu kwa njia hii, ili kuona kama wao watafanya mambo yote yale ambayo Bwana Mungu wao atawaamuru.’ Mwokozi alitangaza: ‘Kwani wote watakaopata baraka mikononi mwangu wataitii sheria iliyowekwa kwa ajili ya baraka hiyo, na masharti yake, kama yalivyowekwa tangu kabla ya kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu.’ Hamna mfano mkuu wa utiifu uliopo kushinda ule wa Mwokozi wetu. Kuhusu Yeye, Paulo alisema: ‘Ingawa alikuwa Mwana, alijifunza kutii kwa mateso hayo yaliyompata; naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii.”
Obedience Brings Blessings, April 2013 general conference
Rais Gordon B. Hinckley
“Ninatoa ushuhuda wangu kwamba furaha ya Watakatifu wa Siku za Mwisho, amani ya Watakatifu wa Siku za Mwisho, maendeleo ya Watakatifu wa Siku za Mwisho, ufanisi wa Watakatifu wa Siku za Mwisho, na wokovu wa milele na kuinuliwa kwa watu hawa kunategemea katika kutembea kwa utiifu kwenye ushauri wa ukuhani wa Mungu.”
If Ye Be Willing and Obedient, October 1971 general conference
Rais James E. Faust
“Utiifu huongoza kwenye uhuru wa kweli. Kadiri tunavyotii ukweli uliofunuliwa, ndivyo tunavyozidi kukombolewa. … Kama vile utaratibu ulivyotoa uhai na uzuri kwa dunia wakati ilikuwa giza na tupu, ndivyo ilivyo kwetu. Utiifu hutusaidia kukuza uwezo kamili ambao Baba yetu wa Mbinguni anatamani kwa ajili yetu katika kuwa viumbe wa selestia wanaostahili siku moja kuishi katika uwepo Wake.”
Obedience: The Path to Freedom, April 1999 general conference
Mzee Jeffrey R. Holland
“Utiifu siyo tu ni sheria ya pekee ya kwanza ya mbinguni. Utiifu ni sheria ya kwanza ya kila kitu. Kila kitu ninachojua ambacho kina umuhimu huitaji nia ya awali ya dhati ya kutii neno na mapenzi ya Bwana. Ni agano la kwanza tunalofanya katika hekalu.”
Elder Jeffrey R. Holland Visits Philippines, Shares Message on Love, Newsroom.ChurchofJesusChrist.org
Mzee L. Tom Perry
“Kwanza, tunatakiwa kuwa watiifu wa sheria za Bwana. Hii ni moja ya masomo ya kwanza yaliyofundishwa kwa Adamu na Hawa: utii huleta imani. Huleta baraka za mbinguni. Kutotii huleta maumivu ya moyo na kukata tamaa. Kufuata sheria ya utii kunahitaji kujitoa wenyewe katika huduma kwa watoto wa Baba yetu wa Mbinguni. Kujitolea kile tulichonacho ili kuwanufaisha kaka na dada zetu ni mtihani mkuu katika injili. Moja ya madhumuni ya uzoefu wa maisha ya duniani ni kuona kama tutafuata ushauri wa Mwokozi wa tafuteni kwanza ninyi ufalme wa Mungu, na utakatifu wake; na vitu vyote mtaongezewa’ [ona Mathayo 6:33].”
Behold, the Lord Hath Shown unto Me Great and Marvelous Things, October 1992 general conference
Mzee Joseph B. Wirthlin
“Sote tunataka mfanikiwe katika maisha haya na kustahili zawadi kubwa zaidi za Mungu—uzima wa milele katika ufalme wa selestia. Ili kufikia malengo yenu katika maisha haya ya duniani na kujithibitisha wenyewe kuwa mnastahili baraka za milele, jifunze kutii. Hakuna njia nyingine. Utiifu huleta nguvu kubwa na uwezo katika maisha yako.”
Live in Obedience, April 1994 general conference
Sheria ya Dhabihu
Rais Russell M. Nelson
“Bado tunaamriwa kutoa dhabihu, lakini si kwa kumwaga damu ya wanyama. Hisia yetu ya juu ya dhabihu inafikiwa pale tunapojiweka kuwa watakatifu zaidi. Tunafanya hivi kwa kutii amri za Mungu. Kwa hivyo, sheria za utii na dhabihu zinaingiliana kwa njia isiyofutika. Fikiria amri za kutii Neno la Hekima, kushika siku ya Sabato kitakatifu, kulipa zaka kwa uaminifu. Tunapotii amri hizi na zingine, kitu kizuri kinatutokea. Tunakuwa na nidhamu! Tunakuwa wafuasi! Tunakuwa watukufu na watakatifu zaidi—kama Bwana wetu!”
Lessons from Eve, October 1987 general conference
Rais Harold B. Lee
“Mpango wetu wa sasa wa ustawi unaweza kuwa mazoezi ya ‘kupanga’ kuona jinsi kanisa hili lilivyo tayari kuishi mpango huu, ili, kama ilivyokuwa utambuzi wa furaha wa watu katika bara hili, kama ilivyoandikwa katika maandiko ya kale tuyaitayo Kitabu cha Mormoni, baada ya wote kuongoka kwa Bwana, ‘hakukuwa na matajiri na maskini, wafungwa na huru, lakini wote walikuwa … washiriki wa karama ya mbinguni’ na ‘hakika hakungekuwa na watu wenye furaha zaidi’ juu ya uso wa dunia (4 Nefi 1:3, 16) kwa kuishi kikamilifu sheria ya dhabihu na kuweka wakfu.”
Teach the Gospel of Salvation, October 1972 general conference
Rais M. Russell Ballard
“Kwa kawaida, jambo la kwanza watu hufikiria wanaposikia ‘sheria ya Musa’ ni dhabihu ya wanyama. Hali ya kutisha ya dhabihu ya damu imesababisha wengine kuuliza, ‘Ni kwa jinsi gani shughuli kama hiyo inaweza kuwa na uhusiano wowote na injili ya upendo?’ Tunaweza kuelewa vizuri zaidi jibu la swali hilo tunapoelewa madhumuni mawili makuu ya sheria ya dhabihu. Madhumuni haya yalitumika kwa Adamu, Ibrahimu, Musa na Mitume wa Agano Jipya, na yanatuhusu leo tunapokubali na kuishi sheria ya dhabihu. Madhumuni yake makuu mawili ni kutujaribu na kututhibitisha na kutusaidia katika kwenda kwa Kristo.”
The Law of Sacrifice, Liahona, March 2002
Mzee L. Tom Perry
“Je, ni ajabu kwamba Bwana, tangu mwanzo, alitaka kuweka mpango wake imara katika akili za watoto wake hapa duniani? Miongoni mwa sheria zilizotolewa kwa Adamu na Hawa, sheria ya dhabihu ilianzishwa kuwakumbusha tukio kubwa ambalo lingetokea katika wakati wa meridiani. … Tangu wakati huo na kuendelea hadi Mwokozi alipokuja duniani, wakati wowote ukuhani ulipokuwepo, mwanadamu alitoa dhabihu ili kumkumbusha wakati ambao Mwana wa Adamu angekuja duniani ili kutoa dhabihu kuu kwa ajili yetu sote.”
Sacrament of the Lord’s Supper, April 1996 general conference
Mzee Neal A. Maxwell
“Sadaka ya kweli na ya kibinafsi kamwe haikuwa kuweka mnyama kwenye madhabahu. Badala yake, ni utayari wa kumuweka kwenye madhabahu mnyama aliye ndani yetu na kumuacha ateketee! Hiyo ni ‘dhabihu kwa Bwana … ya moyo uliovunjika na roho iliyopondeka,’ (Mafundisho na Maagano 59:8), sharti la kuchukua msalaba, wakati ‘tukiacha dhambi [zetu] zote’ ili ‘kumjua Mungu’ (Alma 22:18) kwani kwa kujikana wenyewe ni mwanzo wa kumkubali Yeye.”
Deny Yourselves of All Ungodliness, April 1995 general conference
Sheria ya Injili
Rais Russell M. Nelson
“Kama waumini wa Kanisa, wewe na mimi tunashiriki katika ‘njia ya Bwana mwenyewe.’ Angalau mara moja kwa mwezi, tunafunga na kuomba na kuchangia matoleo ya ukarimu ambayo huwawezesha maaskofu kutoa misaada. Hii ni sehemu ya sheria ya injili. Kila mmoja wetu anaweza kuwasaidia maskini, sasa na kokote walipo. Na sisi, pia, tutabarikiwa na kulindwa kutokana na uasi kwa kufanya hivyo.”
In the Lord’s Own Way, April 1986 general conference
Rais Ezra Taft Benson
“Tunaahidi kuishi sheria ya injili. Sheria ya injili inakumbatia sheria, kanuni na maagizo yote muhimu kwa ajili ya kuinuliwa kwetu. Tunakubali kuonyesha imani katika Yesu Kristo na toba ya kweli inayotokana na moyo uliovunjika na roho iliyopondeka. Tunapotii ibada za ubatizo na uthibitisho, na kuendelea katika imani na maombi, nguvu ya dhabihu ya upatanisho ya Mwokozi inashughulikia dhambi zetu na tunatakaswa udhalimu wote. … Sheria ya injili ni zaidi ya kuelewa mpango wa wokovu. Inajumuisha kushiriki ibada na nguvu za kuunganisha kunakopelekea mtu kuunganishwa katika uzima wa milele. ‘Kuzaliwa mara ya pili,’ alisema Nabii Joseph Smith, ‘huja kwa Roho wa Mungu kupitia ibada.’”
Teachings of Ezra Taft Benson, 337
Rais John Taylor
“Lakini ilikuwa muhimu kwamba Adamu atii, aishi, na kushika sheria ya injili, na pia ilikuwa muhimu kwamba uzao wake, ambao nao wangefikia kuinuliwa na kupokea baraka sawa, pia wangepaswa kushika na kuishi sheria hiyo hiyo.”
The Gospel Kingdom, 279
Rais Wilford W. Woodruff
“Wale wote wanaofuata kanuni za injili ya Kristo wataokolewa kupitia hizo. Anayefuata sheria atalindwa kutokana na hiyo. Mtu yeyote anayetii sheria ya injili ataokolewa na kupokea kuinuliwa na utukufu kupitia hiyo.”
The Discourses of Wilford Woodruff, 22
Mzee Bruce R. McConkie
“Katika uchambuzi wa mwisho, injili ya Mungu imeandikwa, si katika barua zilizokufa za kumbukumbu za maandiko, bali katika maisha ya Watakatifu. Haijaandikwa kwa kalamu na wino kwenye karatasi ya kutengenezwa na mwanadamu, bali kwa mambo na vitendo katika kitabu cha uzima cha kila mtu aliyeamini na mtiifu. Imechorwa katika mwili na mifupa na uwezo wa wale wanaoishi sheria ya selestia, ambayo ni sheria ya injili. Ipo hapo kusomwa na wengine, kwanza, na wale ambao, wakiona matendo mema ya Watakatifu, watajibu kwa kumtukuza Baba yetu aliye mbinguni (ona Mathayo 5:16) na hatimaye kwa Jaji Mkuu ambaye kwake maisha ya kila mtu ni kitabu wazi.”
Our Gospel Came Not Unto You in Word Only…, October 1968 general conference
Sheria ya Usafi wa Kimwili
Rais Russell M. Nelson
“Njia ya Mwokozi ya maisha ni nzuri. Njia yake ni pamoja na usafi wa kimwili kabla ya ndoa na uaminifu kamili ndani ya ndoa. Njia ya Bwana ndiyo njia pekee ya sisi kupata furaha ya kudumu. Njia yake huleta faraja endelevu kwa roho zetu na amani ya kudumu kwenye nyumba zetu. Na bora zaidi, njia Yake inatuongoza nyumbani Kwake na kwa Baba yetu wa Mbinguni, kwenye uzima wa milele na kuinuliwa. Hichi ndicho kiini cha kazi na utukufu wa Mungu.”
Decisions for Eternity, October 2013 general conference
Rais Dallin H. Oaks
“Uwezo wa kuumba maisha ni uwezo wa kutukuka ambao Mungu amewapa watoto Wake. Matumizi yake yaliamriwa na amri ya kwanza ya Mungu kwa Adamu na Hawa (ona Mwanzo 1:28), lakini amri nyingine muhimu zilitolewa ili kukataza matumizi mabaya (ona Kutoka 20:14; 1 Wathesolanike 4:3). HuoMmsisitizo tunaouweka katika sheria ya usafi wa kimwili umeelezewa kwa uelewa wetu wa umuhimu wa mamlaka ya uumbaji katika kukamilisha mpango wa Mungu.Nje ya uhusiano wa ndoa kati ya mwanamume na mwanamke, matumizi yoyote ya uwezo huu ni dhambi na ni kinyume na mpango wa Mungu kwa ajili ya utukufu wa watoto Wake.”
No Other Gods, October 2013 general conference
Mzee David A. Bednar
“Ninaahidi kwamba utii wa sheria ya usafi wa kimwili utaongeza furaha yetu katika maisha ya duniani na kuwezesha maendeleo yetu katika umilele. Usafi wa kimwili na maadili vimekuwa kwa sasa, daima vimekuwa, na daima vitakuwa ‘ni vya thamani sana kuliko vitu vyote’ (Moroni 9:9).”
We Believe in Being Chaste, April 2013 general conference
Mzee Neil L. Andersen
Kuna watu wazima wengi Kanisani ambao wamepita miaka yao ya awali ya utu uzima. Wakati wakikuta maisha yao ya sasa tofauti na walivyotarajia, wanatii sheria ya usafi wa kimwili. Inaweza kuwa ni jaribio la imani yao. Ninatoa heshima yangu ya kina na pongezi kwa wanafunzi hawa wa Kristo.”
Trial of Your Faith, October 2012 general conference
Familia: Tangazo kwa Ulimwengu
“Amri ya kwanza ambayo Mungu aliwapa Adamu na Hawa ilihusiana na uwezo wao wa uzazi kama mume na mke. Tunatangaza kwamba amri ya Mungu kwa watoto Wake ya kuzaana na kujaza dunia imebaki ikizingatiwa. Tunatangaza tena kwamba Mungu ameamuru kwamba nguvu takatifu za kuzaa ni lazima zitumike tu, kati ya mwanamume na mwanamke, ambao wameoana kihalali kama mme na mke. Tunatangaza njia ambayo maisha ya dunia yanaumbwa imechaguliwa kitakatifu. Tunathibitisha utakatifu wa uhai na umuhimu wake katika mpango wa milele wa Mungu.”
Familia: Tangazo kwa Ulimwengu
Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana
“Unapokuwa msafi kimaadili, unajiandaa kufanya na kushika maagano matakatifu hekaluni. Unajitayarisha kujenga ndoa imara na kuleta watoto ulimwenguni kama sehemu ya familia ya milele na yenye upendo. Unajikinga kutokana na uharibifu wa kiroho na kihisia ambao huja kwa kushiriki urafiki wa kujamiiana nje ya ndoa. Unajikinga pia dhidi ya magonjwa hatari. Kubaki msafi kimwili hukusaidia kuwa na ujasiri na furaha ya kweli na huboresha uwezo wako wa kufanya maamuzi mazuri sasa na baadaye. Kiwango cha Bwana kuhusu usafi wa kimwili ni dhahiri na kisichobadilika. Usiwe na mahusiano yoyote ya kimwili kabla ya ndoa, na kuwa mwaminifu kikamilifu kwa mwenzi wako baada ya ndoa. … Usishiriki katika majadiliano au mawasiliano yoyote yanayoamsha hisia za kujamiana. Usishiriki katika aina yoyote ya ponografia.”
Sheria ya Kuweka Wakfu
Rais Ezra Taft Benson
“Tunaweka maagano ya kuishi sheria ya kuweka wakfu. Sheria hii ni kwamba tunaweka wakfu wakati wetu, talanta, nguvu, mali na pesa kwa ajili ya kujenga ufalme wa Mungu hapa duniani na kuijenga Sayuni. Kama mtu hajaishi kwa sheria za utii, dhabihu, injili na usafi wa kimwili, hawezi kufuata sheria ya kuwekwa wakfu, ambayo ni sheria inayohusiana na ufalme wa selestia. “Kwani kama mnataka kwamba niwape mahali katika ulimwengu wa selestia, lazima mjitayarishe wenyewe kwa kufanya mambo niliyo waamuru na ninayoyataka kutoka kwenu ninyi (M&M 78:7).”
Teachings of Ezra Taft Benson, 121
Rais Spencer W. Kimball
“[Tu]naweka wakfu wakati wetu, talanta na tulivyo navyo kama itakavyohitajika na viongozi wetu na kama inavyochochewa na minong’ono ya Roho. Katika Kanisa, kama ilivyo katika mfumo wa Ustawi pia, tunaweza kutoa maelezo kwa kila uwezo, kila hamu ya haki, kila msukumo wa kufikiria. Iwe ni mtu wa kujitolea, baba, mwalimu wa nyumbani, askofu au jirani, iwe mwalimu anayetembelea, mama, mtunza nyumba au rafiki—kuna nafasi kubwa ya kutoa vyote tulivyonavyo. Na tunapotoa, tunaona kwamba ‘dhabihu huleta baraka za mbinguni!’ (Nyimbo za Dini, na. [17]) Na mwishoni, tunajifunza kuwa haikuwa dhabihu hata kidogo.”
Becoming the Pure in Heart, April 1978 general conference
Mzee D. Todd Christofferson
“Maisha yetu hapa duniani ni usimamizi wa wakati na chaguzi yaliyotolewa na Muumba wetu. Neno usimamizi linakumbusha sheria ya Bwana ya kuweka wakfu (ona, kwa mfano, Mafundisho na Maagano 42:32, 53), ambayo ina jukumu la kiuchumi lakini, zaidi ya hayo, ni matumizi ya sheria ya selestia katika maisha haya na sasa (ona Mafundisho na Maagano 105:5). Kuweka wakfu ni kukitenga rasmi kitu au kukifanya kitu kuwa kitakatifu, kilichowekwa kwa madhumuni yaliyo matakatifu. Mafanikio ya kweli katika maisha haya huja kwa kuyaweka wakfu maisha yetu—hayo ni pamoja na, muda wetu na uchaguzi wetu—kwa malengo ya Mungu (ona Yohana 17:1,4; Mafundisho na Maagano 19:19). Kwa kufanya hivyo, tunamruhusu Yeye kutuinua kwenye hatima yetu ya juu.”
Reflections on a Consecrated Life, October 2010 general conference
Mzee Neal A. Maxwell
“Mara nyingi tunafikiri kuweka wakfu ni kama kuitikia, kutoa mali yetu wakati tunapoongozwa kiungu kufanya hivyo Lakini hatma kuu ya kuweka wakfu ni kujitoa sisi binafsi kwa Mungu. Moyo, nafsi na akili vilikuwa maneno ya Kristo yaliyozunguka katika kuelezea amri ya kwanza, ambayo daima, sio mara kadhaa, ni ya utendaji (ona Mathayo 22:37). Ikiwa tutaitii, basi utendaji wetu, kama matokeo, utawekwa wakfu kikamilifu kwa ustawi wa kudumu wa nafsi zetu (ona 2 Ne. 32:9).”
Consecrate thy Performance, April 2002 general conference
Rais Henry B. Eyring
“Baba yetu wa Mbinguni anasikia maombi ya watoto wake duniani kote… Maombi hayo yamemfikia tangu alipowaweka waume na wake ulimwenguni.
Kwa sababu Bwana husikia kilio chao na kuhisi huruma yako kwao, Yeye tangu mwanzo wa nyakati ametoa njia kwa wafuasi wake kusaidia. Amewaalika watoto Wake kuweka wakfu wakati wao, mali yao na nafsi zao ili kuungana naye katika kuwahudumia wengine. Njia yake ya kuwasaidia wakati mwingine huitwa kuishi maisha ya kuweka wakfu.”
Opportunities to Do Good, April 2011 general conference
Mzee David A. Bednar
“Kuweka wakfu uhusiana na hujenga juu ya dhabihu. Neno wakfu linamaanisha kuendeleza na ‘kujitolea kwa kusudi takatifu.’ Dhabihu ni kile tutakachotoa, kusalimisha, kutoa au kuachana nacho. Wakfu, kwa upande mwingine, ni kuendeleza kikamilifu na kujitolea kwa kusudi takatifu. … Tunapoishi sheria ya kuweka wakfu, tuko tayari sio tu kutoa chochote na kila kitu ambacho tunamiliki kwa ajili ya injili—lakini pia tunaahidi kujikuza na kujitoa sisi wenyewe—muda wetu, talanta zetu na uwezo wetu unaoongezeka kila wakati—kwa ajili ya ujenzi wa ufalme wa Mungu duniani. Ahadi yetu ni: Nitajitolea mimi na yote niwezayo kuwa, na nitaishi kwa ajili ya injili ya Yesu Kristo. Kanuni ya dhabihu ni sheria ndogo ya maandalizi kwa ajili ya kanuni ya kuweka wakfu. Kuweka wakfu hujumuisha na ni pamoja na dhabihu na mengi zaidi. … Kuweka wakfu huchochewa na hisani na huzalisha ongezeko zaidi la hamu ya kutumikia. Katika siku hizi za mwisho, sisi tunahitajika zaidi kama watoto wa agano kuliko pesa zetu, vitu na wakati. Tunahitaji kuweka wakfu kwa Bwana roho zetu zote.”
Adapted from a devotional address given at BYU-Idaho, “Your Whole Souls as an Offering Unto Him,” David A. Bednar, January 5, 1999
Kuunganisha
Rais Russell M. Nelson
“Kaka na dada, mali za kimwili na heshima za ulimwengu hazidumu. Lakini muungano wako kama mke, mume na familia unaweza kudumu. Muda pekee wa maisha ya familia ambao unakidhi hamu kubwa ya mwanadamu ni milele. Hakuna dhabihu iliyo kubwa zaidi kuliko kuwa na baraka za ndoa ya milele. Ili kustahili, mtu anahitaji tu kujikana mwenyewe kutoka vitu visivyompendeza Mungu na kuheshimu ibada za hekaluni. Kwa kufanya na kushika maagano matakatifu ya hekaluni, tunathibitisha upendo wetu kwa Mungu, kwa mwenzi wetu na heshima yetu halisi kwa uzao wetu—hata wale ambao bado hawajazaliwa. Familia yetu ni fokasi ya kazi yetu kubwa na furaha katika maisha haya; hivyo itakuwa milele yote, wakati tutakapoweza ‘kurithi viti vya enzi, falme, uwezo, … nguvu, utawala, … kuinuliwa na utukufu.’ Baraka hizi zipatikanazo bure zinaweza kuwa zetu ikiwa tutaweka nyumba zetu kuwa za utaratibu sasa na kwa uaminifu kushikilia injili.”
Set in Order Thy House, October 2001 general conference
Rais Dallin H. Oaks
“Lengo la Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho ni kuwasaidia watoto wote wa Mungu kuelewa uwezekano wao wa kuwa na kupata hatima yao ya juu kabisa. Kanisa hili linaishi ili kutoa kwa wana na mabinti wa Mungu njia ya kuingia ndani ya na kuinuliwa katika ufalme wa selestia. Hili ni kanisa linalozingatia familia katika mafundisho na matendo. Uelewa wetu wa asili na kusudi la Mungu Baba wa Milele unaelezea hatima yetu na uhusiano wetu katika familia yake ya milele. Thiolojia yetu huanza na wazazi wa mbinguni. Matarajio yetu ya juu ni kuwa kama wao. Chini ya mpango wa huruma wa Baba, haya yote yanawezekana kupitia upatanisho wa Mzaliwa wa Pekee wa Baba, Bwana wetu na Mwokozi, Yesu Kristo. Kama wazazi wa kidunia tunashiriki katika mpango wa injili kwa kutoa miili ya kufa kwa ajili ya watoto wa kiroho wa Mungu. Utimilifu wa wokovu wa milele ni jambo la familia.”
Apostasy and Restoration, April 1995 general conference
Rais Henry B. Eyring
“Kila kitu tunachofanya chapaswa kuwa na ndoa ya selestia kama kitovu na lengo lake. Hiyo ina maana kuwa ni lazima tujitahidi kuunganishwa na mwenza wa milele katika hekalu la Mungu. Lazima pia tuwahimize wengine kufanya na kutii maagano ambayo yanawaunganisha mume na mke pamoja, pamoja na familia yao, katika maisha haya na ulimwengu ujao.”
Familia ya Milele, mkutano mkuu wa Aprili 2016
Rais Boyd K. Packer
“Mwisho wa shughuli zote katika Kanisa ni kuona mume na mke wake na watoto wao wakiwa na furaha nyumbani, wakilindwa na kanuni na sheria za injili, wakifungwa salama katika maagano ya ukuhani usio na mwisho.”
And a Little Child Shall Lead Them, April 2012 general conference
Rais Dieter F. Uchtdorf
“Ninashukuru kwamba mimi ni wa kanisa ambalo linathamini ndoa na familia. Waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho wanajulikana ulimwenguni kote kwa kuwa na baadhi ya ndoa na familia zilizo nzuri sana mnazoweza kuzipata duniani. Naamini hii ni kwa sababu, kwa kiasi fulani, kwa sababu ya ukweli wa thamani uliorejeshwa kupitia Joseph Smith kwamba ndoa na familia zilikusudiwa kuwa za milele. Familia hazipo tu ili kufanya mambo yaende vizuri hapa duniani na kisha kutupwa tunapofika mbinguni. Bali, ni utaratibu wa mbinguni. Ni mwangwi wa mpangilio wa kiselestia na mfano wa familia ya milele ya Mungu.”
Katika Kuwasifu Wale Wanaookoa, mkutano mkuu wa Aprili 2016
“Familia: Tangazo kwa Ulimwengu”
“Mpango mtakatifu wa furaha unawezesha uhusiano wa familia kuendelezwa zaidi ya kaburi. Maagizo na maagano matakatifu yanayopatikana katika mahekalu matakatifu yanawezesha watu binafsi kurudi katika uwepo wa Mungu na kwa familia kuunganishwa milele.”
Baraka za Kuabudu Hekaluni
Rais Russell M. Nelson
Kila binadamu anayekuja hapa duniani ni zao la vizazi vya wazazi. Tuna hamu ya asili ya kuungana na mababu zetu. Hamu hii inakaa katika mioyo yetu, bila kujali umri. Fikiria uhusiano wa kiroho ambao huundwa wakati msichana anamsaidia bibi yake kuingiza habari za familia kwenye kompyuta au wakati kijana anaona jina la baba wa babu yake kwenye rekodi ya sensa. Wakati mioyo yetu inageuka kwa mababu zetu, kitu kinabadilika ndani yetu. Tunahisi sehemu ya kitu kikubwa kuliko sisi wenyewe. Matamanio yetu ya kuzaliwa kwa uhusiano wa familia yanatimizwa tunapounganishwa na mababu zetu kupitia ibada takatifu za hekalu.”
Generations Linked in Love, April 2010 general conference
Rais Thomas S. Monson
“Kwa nini wengi wako radhi kutoa sana ili kupokea baraka za hekaluni? Kwa wale wanaoelewa baraka za milele zinazotokana na Hekalu wanajua kuwa hakuna kujitolea kuliko kukuu, hakuna gharama iliyo ghali wala mapambano yaliyo magumu ili kupokea baraka hizo. Hakuna kamwe maili nyingi sana za kusafiri, vizuizi vingi vya kushinda na shida nyingi ya kuvumilia. Wanaelewa kuwa ibada okozi zinazopokelewa hekaluni siku moja zitatuwezesha kurudi kwa Baba yetu wa Mbinguni katika uhusiano wa familia ya milele na kutunukiwa baraka na nguvu kutoka juu zinastahili kila dhabihu na kila jitihada.”
The Holy Temple—A Beacon to the World, April 2011 general conference
Rais Gordon B. Hinckley
“Ninaamini kwamba hakuna muumini wa Kanisa aliyepokea mwisho ambao Kanisa hili linapaswa kutoa mpaka apokee baraka zake za hekaluni katika nyumba ya Bwana.”
Some Thoughts on Temples, Retention of Converts, and Missionary Service, October 1997 general conference
Rais Howard W. Hunter
“Katika roho hiyo ninawaalika Watakatifu wa Siku za Mwisho kutegemea hekalu la Bwana kama ishara kubwa ya uumini wako. Ni shauku ya ndani kabisa ya moyo wangu kuona kila muumini wa Kanisa anastahili kuingia hekaluni. Itamfurahisha Bwana kama kila muumini mtu mzima atastahili—na kubeba—kibali hai cha hekaluni. Mambo ambayo tunapaswa tufanye na tusifanye ili kustahili kibali cha hekaluni ni mambo yale yale yanayohakikisha tutakuwa na furaha kama watu binafsi na kama familia. Tuweni watu wanaohudhuria hekaluni. Huhudhurieni hekaluni mara nyingi kulingana na hali binafsi zinavyoruhusu. Weka picha ya hekalu katika nyumba yako ili kwamba watoto wenu waione. Wafundishe kuhusu madhumuni ya nyumba ya Bwana. Wafanye wapange kutoka miaka yao ya mapema kwenda huko na kubaki kuwa wastahiki wa baraka hiyo.”
Exceeding Great and Precious Promises, October 1994 general conference
Mzee David A. Bednar
“Roho ya Eliya inaathiri watu ndani na nje ya Kanisa. Hata hivyo, kama waumini wa Kanisa la Kristo lililorejeshwa, tuna jukumu la agano la kuwatafuta mababu zetu na kufanya maagano ya kuokoa ya Injili kwa ajili yao. ‘Wao pasipo sisi hawakamilishwi (Waebrania 11:40; ona pia Mafundisho: Joseph Smith, 475). Na ‘wala sisi hatuwezi kuwa wakamilifu pasipo wafu wetu (Mafundisho na Maagano 128:15). Kwa sababu hizi tunafanya utafiti wa historia ya familia, kujenga mahekalu na kufanya ibada za uwakilishi. Kwa sababu hizi Eliya alitumwa ili kurejesha mamlaka ya kuunganisha ambayo huunganisha duniani na mbinguni. Sisi ni mawakala wa Bwana katika kazi ya wokovu na kuinuliwa ambayo itazuia ‘dunia yote [isipigwe] kwa laana’ (Mafundisho na Maagano 110:15) atakaporudi tena. Hii ndiyo kazi yetu na baraka kubwa.
The Hearts of the Children Shall Turn, October 2011 general conference
Mzee Quentin L. Cook
“Mafundisho ya familia kuhusiana na historia ya familia na kazi ya hekalu yapo wazi. Bwana katika maagizo ya awali ya ufunuo alitaja ‘ubatizo kwa niaba ya wafu wako.’ Wajibu wetu wa mafundisho ni kwa mababu zetu wenyewe. Hii ni kwa sababu mpangilio wa selestia wa mbinguni unategemea familia. Urais wa Kwanza umewahimiza waumini, hasa vijana na vijana wasio na ndoa, kusisitiza kazi ya historia ya familia na ibada kwa ajili ya majina ya familia zao wenyewe au majina ya mababu wa kata zao na waumini wa kigingi. Tunahitaji kuunganishwa na mizizi yetu na matawi. Wazo la kuwa na uhusiano katika ulimwengu wa milele kwa kweli ni tukufu.”
Roots and Branches, April 2014 general conference
Rais Boyd K. Packer
“Haijalishi uraia au rangi gani, awe wa kiume au wa kike, bila kujali kazi gani, bila kujali elimu yako, bila kujali kizazi ambacho mtu anaishi, maisha ni safari ya kurudi nyumbani kwetu sote, kurudi kwenye uwepo wa Mungu katika ufalme wake wa selestia. Ibada na maagano yanakuwa ni sifa zetu kwa ajili ya kukubaliwa kwenye uwepo Wake. Kuzipokea kwa kustahili ni kiu ya maisha yote; kuzitii baada ya hapo ni changamoto ya maisha haya. Mara tu tutakapozipokea kwa ajili yetu wenyewe na kwa ajili ya familia zetu, tunalazimika kutoa ibada hizi kwa ajili ya jamaa zetu waliofariki, kwa kweli kwa familia nzima ya binadamu.”
Covenants, Ensign, May 1987