Maandiko Matakatifu
Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko kwa Familia Yako


“Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko kwa Familia Yako,” Mawazo ya Kujifunza Maandiko (2021)

“Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko kwa Familia Yako,” Mawazo ya Kujifunza Maandiko

Picha
familia zikijifunza maandiko

Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko kwa Familia Yako

Kujifunza maandiko kwa familia kila mara ni njia yenye nguvu zaidi katika kuisaidia familia yako kujifunza injili. Ni kiasi gani na kwa muda gani mnasoma kama familia siyo muhimu kama vile kuwa thabiti katika jitihada zenu. Unapofanya kujifunza maandiko kuwa sehemu muhimu ya maisha ya familia yako, utawasaidia wanafamilia yako kuja karibu na Yesu Kristo na kujenga shuhuda zao juu ya msingi wa neno Lake.

Zingatia maswali yafuatayo:

  • Je, ni kwa jinsi gani unaweza kuwatia moyo wanafamilia kusoma maandiko peke yao?

  • Je, unaweza kufanya nini ili kuwatia moyo wanafamilia kushiriki kile wanachojifunza?

  • Je, ni kwa jinsi gani unaweza kusisitiza kanuni unazojifunza katika maandiko kwenye nyakati za kila siku za kufundisha?

Kumbuka kwamba nyumbani ni mahali bora pa kujifunza na kufundisha injili. Unaweza kujifunza na kufundisha injili nyumbani katika njia ambazo haziwezekani katika darasa la Kanisani. Kuwa mbunifu unapofikiria njia za kuisaidia familia yako kujifunza kutoka kwenye maandiko. Zingatia baadhi ya mawazo yafuatayo ili kuboresha kujifunza maandiko kwa familia yako.

Tumia Muziki

Imbeni nyimbo zinazoimarisha kanuni zinazofundishwa katika maandiko.

Picha
mwanamume na msichana wakijifunza maandiko

Shiriki Maandiko Yenye Maana Zaidi

Wape wanafamilia muda wa kushiriki vifungu vya maandiko ambavyo wameona vina maana zaidi wakati wa kujifunza kwao binafsi.

Tumia Maneno Yako Mwenyewe

Waalike wanafamilia kufanya muhtasari kwa maneno yao wenyewe kile wanachojifunza kutoka kwenye maandiko mnayojifunza.

Tumia Maandiko katika Maisha Yako

Baada ya kusoma kifungu cha maandiko, waalike wanafamilia kushiriki jinsi kifungu hicho kinavyohusiana na maisha yao.

Uliza Swali

Waalike wanafamilia waulize swali la injili, na kisha watumie muda kutafuta mistari inayoweza kusaidia kujibu swali hilo.

Onyesha Andiko

Chagua mstari unaoona una maana, na ubandike mahali ambapo wanafamilia watauona mara kwa mara. Waalike wanafamilia wafanye zamu ya kuchagua andiko la kubandika.

Tengeneza Orodha ya Maandiko

Kama familia, chagueni mistari kadhaa ambayo mngependa kuijadili wiki inayofuata.

Kariri Maandiko

Chagua kifungu cha maandiko ambacho kina maana kwa familia yako, na waalike wanafamilia kukikariri kwa kukirudia kila siku au kucheza mchezo wa kukariri.

Shiriki Masomo ya Vitendo

Tafuta vitu ambavyo vinahusiana na sura na mistari ambayo mnaisoma kama familia. Waalike wanafamilia kuzungumzia jinsi kila kitu kinavyohusiana na mafundisho katika maandiko.

Picha
mwanamke akimfundisha mtoto

Chagua Mada

Waruhusu wanafamilia kufanya zamu za kuchagua mada ambayo familia itajifunza pamoja. Tumia Mwongozo wa Mada, Kamusi ya Biblia, au Mwongozo wa Maandiko (scriptures.ChurchofJesusChrist.org) ili kutafuta vifungu vya maandiko kuhusu mada.

Chora picha

Someni mistari michache kama familia, na kisha toa muda kwa wanafamilia kuchora kitu kinachohusiana na kile mnachokisoma. Tumieni muda kujadili mchoro wa kila mmoja.

Igiza Hadithi

Baada ya kusoma hadithi, waalike wanafamilia kuiigiza. Baadaye, zungumzeni kuhusu jinsi hadithi inavyohusiana na mambo mnayopitia kama mtu binafsi na kama familia.

Mzee David A. Bednar alifundisha: “Kila sala ya familia, kila tukio la kujifunza maandiko kwa familia, na kila jioni ya familia nyumbani ni alama kwenye turubai ya roho zetu. Hakuna tukio moja linaloweza kuonekana kuwa la kuvutia sana ama la kukumbukwa. Lakini kama vile tu alama za rangi ya njano na dhahabu na hudhurungi zinavyosaidiana kila moja na kuzalisha kitu bora, hivyo pia uthabiti wetu wa kufanya mambo yanayoonekana kuwa madogo madogo unaweza kusababisha matokeo muhimu ya kiroho” (“Bidii Zaidi na Kuhusika Nyumbani,” Liahona, Nov. 2009, 19–20).