“Wewe ni Mtoto wa Thamani wa Mungu,” Maendeleo Binafsi: Kitabu cha Mwongozo kwa Vijana (2019)
“Wewe ni Mtoto wa Thamani wa Mungu,” Maendeleo Binafsi: Kitabu cha Mwongozo kwa Vijana
Wewe ni Mtoto wa Thamani wa Mungu
Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo waliumba vitu vyote, wanajua vitu vyote, na wameshinda vitu vyote. Na Wanataka uwe kama Wao! Unapofanya maagano na kufuata mpango wa Mungu, unaweza kutumia karama zako za kipekee kukua na kuwatumikia wengine.
Unaweka agano kumfuata Yesu Kristo wakati unapobatizwa na unapopokea sakramenti.
Unapothibitishwa, unapokea kipawa cha Roho Mtakatifu ili akuongoze.
Unaweza kushiriki katika kazi ya Mungu na kuhudumu Kanisani chini ya mamlaka ya funguo za ukuhani.
Unaweza kujifunza na kukua unaposoma, unapoishi, na kushiriki injili.
Unaweza kupata furaha wakati unapowapenda na kuwahudumia wengine kama Yesu alivyofanya.
Baba wa Mbinguni alimtuma Mwana Wake, Yesu Kristo, kuwa mfano kamili na kufanya iwezekane kwako kutubu na kubadilika.
Hekaluni, unaweza kuhudumu na kufanya maagano ambayo yanawaunganisha watoto wa Mungu milele.