Agano la Kale 2022
Machi 14–20. Mwanzo 42–50: “Mungu Alimaanisha kwa Mazuri”


“Machi 14–20. Mwanzo 42–50: ‘Mungu Alimaanisha kwa Mazuri,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano la Kale 2022 (2021)

“Machi 14–20. Mwanzo 42–50,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2022

Picha
Yusufu wa Misri

Mchoro wa Yusufu wa Misri, na Robert T. Barret

Machi 14–20

Mwanzo 42–50

“Mungu Alimaanisha kwa Mazuri”

Ni muhimu kujua maandiko unayofundisha, lakini ni muhimu pia kujua watoto unaowafundisha. Chukua muda kutafakari na kusali kuhusu vyote.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Kwa sababu hadithi katika Mwanzo 42–50 ni mwendelezo wa hadithi katika somo la wiki iliyopita, kutoka Mwanzo 37–41, tumia muda mwanzoni mwa darasa kuwaacha watoto washiriki wanachokumbuka kuhusu Yusufu, pamoja na walivyojifunza kaika Msingi na nyumbani.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Mwanzo 45:4–15

Ninaweza kuonyesha upendo kwa familia yangu

Kwa watoto wadogo, unaweza kutaka kusisitiza sehemu za hadithi hii ambayo Yusufu alionyesha upendo kwa familia yake.

Shughuli Yamkini

  • Tumia “Yusufu na Njaa” (katika Hadithi za Agano la Kale) au picha kutoka Njoo, Unifuate–Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia, waambie watoto kuhusu muunganiko wa Yusufu na kaka zake zake. Sisitiza jinsi Yusufu alivyoonyesha upendo kwa kaka zake zake.

  • Soma kifungu cha maneno kutoka Mwanzo 45:4–15 ambacho kinaelezea mambo ambayo Yusufu alifanya kuonyesha anaipenda familia yake. Waalike watoto kujifanya kutenda kama vile mistari inavyoelezea. Kwa mfano wanaweza kujifanya wanamuuliza mshiriki wa familia “kuja karibu”(mstari wa 4) au kumpa mshiriki wa familia chakula (ona mstari wa 11).

  • Imbeni wimbo kuhusu upendo, kama vile “Jesus Said Love Everyone” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,136). Saidia watoto kuchora kielelezo cha mikono yao na uandike katika kielelezo kitu ambacho wanaweza kufanya kuonyesha upendo kwa familia zao.

Mwanzo 48:8–9

Baraka za Ukuhani zinanisaidia.

Yakobo aliwabariki wanawe na wajukuu zake (ona Mwanzo 48–49). Leo tunaweza kupokea baraka za ukuhani ambazo hutupa faraja, uponyaji, mwongozo, na nguvu ya kiroho.

Picha
mvulana akipokea baraka

Tunaweza kupokea baraka kutoka kwa wale wanaoshikilia ukuhani.

Shughuli Yamkini

  • Waonyeshe watoto picha ya Yakobo akibariki wanawe au picha zingine za baraka za ukuhani (tazama picha kwenye muhtasari huu; ona pia Kitabu cha Sanaa za Injili, na. 12). Waombe watoto kueleza ni nini kinatokea katika picha.

  • Soma kwa watoto Mwanzo 48:8–9. Fafanua kwamba Israeli, anayeitwa pia Yakobo, alikuwa baba wa Yusufu na kwamba alitaka kuwapa watoto wa Yusufu baraka za ukuhani. Ikiwa yeyote kati ya watoto amepokea baraka ya ukuhani, waalike wasimulie kuhusu uzoefu wao. Au shiriki uzoefu wako mwenyewe.

  • Saidia watoto wafikirie sababu ambazo wanaweza kuomba baraka ya ukuhani. Wasaidie pia kuwataja wenye ukuhani ambao wanaweza kuwaomba, kama vile baba, babu, au kaka anayehudumu.

Mwanzo 50:15–21

Mimi Naweza kusamehe.

Je, Watoto wanaweza kujifunza nini kuhusu msamaha kutoka kwa mfano wa Yusufu wa kuwasamehe kaka zake zake?

Shughuli Yamkini

  • Tumia ukurasa wa shughuli wa wiki hii kuwasaidia watoto kukumbuka jinsi kaka zake wa Yusufu walikuwa hawana huruma. Soma kwa watoto Mwanzo 50:17, ukisisitiza kwamba kaka zake walijuta kwa waliyoyafanya na walitaka Yusufu awasamehe. Soma mstari wa 21 ili kuonyesha kwamba Yusufu aliwasamehe kaka zake —hakuwakasirikia tena.

  • Imbeni pamoja “Help Me, Dear Father” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 99). Unapoimba kuhusu kusamehe, waombe watoto waonyeshe picha ya Yusufu kwenye ukurasa wa shughuli. Unapoimba kuhusu kutubu, waalike waonyeshe picha za kaka zake zake.

  • Wasaidie watoto wafikirie hali ambazo wanaweza kuhitaji kusamehe mtu. Waalike watoto wafanye kile wanachoweza kusema au kufanya kuonyesha msamaha kwa mtu huyo.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Mwanzo 42–44; 45:1–15

Msamaha huleta amani.

kaka zake zake Yusufu walikuwa wamemtendea mambo mabaya. Walakini Yusufu aliwasamehe na kuleta amani kwa familia yake.

Shughuli Yamkini

  • Wasaidie watoto kuigiza matukio kutoka Mwanzo 42–44. Wanapofanya hivyo, waulize jinsi wanavyofikiria Yusufu angehisi kuwaona kaka zake zake tena au jinsi kaka zake wangehisi walipomtambua Yusufu hatimaye.

  • Waulize watoto inamaanisha nini kusamehe mtu. Wasaidie kuelewa kwamba kusamehe mtu ni pamoja na kumtendea kwa upendo kama wa Kristo. Waulize watoto wanajua nini kuhusu hadithi ya Yusufu kuwasamehe kaka zake, au soma na watoto mistari kutoka Mwanzo 45:1–15. Je, Yusufu alifanya nini au kusema ili kuwajulisha kaka zake zake kwamba aliwasamehe? Je, tunaweza kusema au kufanya nini pale wengine wanapotuomba tuwasamehe?

  • Waulize watoto wafikirie wakati ambao walimsamehe mtu au mtu aliwasamehe. Ili kuwapa wakati wa kufikiria, shiriki uzoefu wako mwenyewe, na ushuhudie baraka zilizotokana na msamaha. Waalike watoto kushiriki uzoefu wao, kama wangependa. Walihisi vipi? Je, tunajifunza nini kuhusu msamaha kutoka kwa mfano wa Mwokozi? (ona Luka 23:33–34).

Mwanzo 45:5–11

Baba wa Mbinguni alimtuma Yesu Kristo kuniokoa.

Hadithi ya Yusufu kuokoa familia yake kutokana na njaa inaweza kutufundisha kuhusu Yesu Kristo, ambaye hutuokoa kutoka kwa dhambi na kifo.

Shughuli Yamkini

Tafsiri ya Joseph Smith, Mwanzo 50:27–33 (katika kiambatanisho cha Biblia)

Baba wa mbinguni alimtayarisha Joseph Smith kuwa nabii katika siku zetu.

Maelfu ya miaka ijayo, Yusufu wa Misri aliona kwamba Bwana angemuita Joseph Smith afanye kazi kubwa katika siku za mwisho. Wafundishe watoto jinsi Bwana ametubariki kupitia Nabii Joseph Smith.

Shughuli Yamkini

  • Wape watoto maelezo yanayoelezea kuhusu Joseph Smith, na waalike wafikirie unamuelezea nani. Jumuisha ishara kutoka Joseph Smith Tafsiri, Mwanzo 50:27–33 (katika kiambatisho cha Bibilia), kama vile “alitufundisha kuhusu maagano” (ona mstari wa 28), “alitupa neno la Bwana” (ona mstari wa 30), na “aliitwa jina la baba yake” (see mstari wa 33). Baada ya watoto kubashiri kwa usahihi, waalike kutafuta ishara hizi kwenye msitari. Je, ni nini kingine tunachojifunza kuhusu Joseph Smith kutoka kwa unabii wa Yusufu huko Misiri?

  • Onyesha watoto picha ambazo zinaonyesha vitu muhimu ambavyo Joseph Smith alifanya au kufundisha (ona, kwa mfano, Kitabu cha Sanaa ya Injili, na. 89–95, 97, 98, 117, 118). Wasaidia watoto wafikirie baraka tulizo nazo kwa sababu ya Joseph Smith. Kwa mfano, kazi yake imetusaidiaje kumkaribia Yesu Kristo?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kushiriki ukurasa wa shughuli wa wiki hii na familia zao nyumbani. Wanaweza kuutumia kurejea hadithi ya Yusufu na kaka zake zake na kujadili umuhimu wa upendo na msamaha katika familia zetu.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Shuhudia kuhusu Yesu Kristo. Hata ingawa Agano la Kale halijataja jina la Yesu Kristo, linamrejelea kwa majina mengine, na linamshuhudia Yeye kupitia alama na hadithi. Wasaidie watoto kujifunza kutafuta kweli kuhusu Mwokozi wakati wowote wanaposoma maandiko.