“Ahadi za Ezekieli Zinatimia,” Jumbe za kila Mwezi za gazeti la Rafiki, Oktoba 2022
Ahadi za Ezekieli Zinatimia
Ujumbe wa Kila mwezi wa gazeti la Rafiki, Oktoba 2022
Ahadi za Ezekieli Zinatimia
Vielelezo na Apryl Stott
Ezekieli alikuwa nabii. Mungu alimwonyesha mambo mengi ya siku zijazo ambayo yalikuwa bado hayajatokea. Ezekieli aliyaandika.
Ezekieli aliandika kuhusu vitabu viwili ambavyo vingepigwa chapa siku za baadaye. Kitabu kimoja kilikuwa Biblia. Kitabu kingine kilikuwa Kitabu cha Mormoni.
Miaka mingi baadaye, Biblia ilichapishwa.
Baada ya miaka mingi zaidi, Joseph Smith alitafsiri Kitabu cha Mormoni. Ono la Ezekieli lilitimia!
Leo tunaweza kusoma kwenye Biblia na Kitabu cha Mormoni. Vitabu hivi vinafanya kazi pamoja kufundisha kuhusu Yesu Kristo.
Ninaposoma maandiko, ninajifunza kuhusu Yesu Kristo
Ukurasa wa Kupaka Rangi
Ninaweza kusoma maandiko
Bofya kwenye picha ili kupakua.
Kielelezo na Apryl Stott
Ni hadithi gani ya maandiko unayoipenda sana?
© 2022 na Intellectual Reserve, Inc. Haki zote zimehifadhiwa. Limepigwa chapa Marekani. Idhini ya Kiingereza: 6/19. Idhini ya kutafsiri: 6/19. Tafsiri ya Monthly Friend Message, October 2022. Swahili. 18317 743