2016
Kutii Amri na Kuwapenda Wengine
Septemba 2016


Vijana

Kutii Amri na Kuwapenda Wengine

Tunapofikiria upendo, mara nyingi kitu cha kwanza kinachokuja akilini mwetu ni sinema za mapenzi, chokoleti na maua. Lakini upendo—kweli upendo—ni wandani zaidi na sio wa kipekee. Yesu Kristo aliishi kwa ajili yetu na alikufa kwa ajili yetu kwa sababu ya upendo Wake kwetu. Kwa kweli, amri kuu mbili ni kumpenda Mungu na kumpenda jirani yetu (ona Mathayo 22:36–40). Lakini tunawezaje kuwaonyesha wengine kwamba tunawapenda?

Rais Uchtdorf anashiriki fumbo la wana wawili, mmoja anayefanya kazi kwa baba yake na mwingine asiyefanya kazi. Mwokozi anatoa mtazamo kwamba mwana aliyemtii baba yake kweli anampenda yeye. Vivyo hivyo, tunapotii amri za Mungu, tunaonyesha kwamba tunampenda na tunataka kurudi Kwake.

Lakini tunawezaje kuonyesha tunampenda kila mtu? Rais Uchtdorf anaelezea hivyo pia: “Kama kweli tunawapenda wenzetu, tunajitoa sisi wenyewe kuwasaidia, maskini na wenye shida, wagonjwa na wanaoteseka.” Kwani wale watendao matendo ya huruma na huduma isiyo ya kibinafsi, hao ndio wafuasi wa Yesu Kristo.

Hivyo wakati mwingine utakapomwona mzazi wako, ndugu, au rafiki, fikiria kuhusu kuwatumikia ili kuonyesha upendo wako kwao. Siyo tu itawafanya kuwa na furaha, lakini itamfanya Baba yako wa Mbinguni awe na furaha pia.