Maandiko Matakatifu
Mafundisho na Maagano 4


Sehemu ya 4

Ufunuo uliotolewa kupitia Joseph Smith Nabii kwa baba yake Joseph Smith Mkubwa, huko Harmony, Pennsylvania, Februari 1829.

1–4, Utumishi wa kishujaa huwaokoa wahudumu wa Bwana; 5–6, Sifa ya uchamungu huwapasisha wao kwenye huduma; 7, Mambo ya Mungu ni lazima yatafutwe.

1 Sasa tazama, akazi ya ajabu karibu yaja miongoni mwa wanadamu.

2 Hivyo basi, ninyi nyote ambao mnaingia katika autumishi wa Mungu, angalieni kwamba bmnamtumikia yeye kwa cmoyo wenu wote, uwezo, akili na nguvu zenu zote, kwamba muweze kusimama pasipo dlawama mbele za Mungu siku ile ya mwisho.

3 Kwa hivyo, kama unayo tamaa ya kumtumikia Mungu wewe aumeitwa kwenye kazi hiyo;

4 Kwani tazama ashamba ni jeupe tayari kwa bmavuno; na lo, yeye aingizaye mundu yake kwa nguvu, ndiye huyo huyo ajiwekeaye cghalani akiba ili asiangamie, bali ajiletee wokovu kwa nafsi yake;

5 Na aimani, btumaini, chisani na dupendo, na ejicho lake likiwa kwenye futukufu wa Mungu pekee, humpasisha mtu huyo katika kazi.

6 Kumbuka imani, awema, maarifa, kiasi, buvumilivu, upendano wa kindugu, uchamungu, hisani, cunyenyekevu, djitihada.

7 aOmba, nawe utapata; bisha, nawe utafunguliwa. Amina.