2018
Nini, Kwa nini, na Jinsi gani: Uainishaji wa Urejesho
April 2018


Nini, Kwa nini, na Jinsi gani: Uainishaji wa Urejesho

Kufundisha injili, utahitajika kuweza kuelezea ukengeufu ni nini, vipindi vya mwongozo wa Mungu, na Urejesho. Chati hii inaweza kusaidia.

Picha
a breakdown of the restoration 1
Picha
a breakdown of the restoration 2

Tuseme uko kwenye safari ya wiki nzima pwani pamoja na familia ya rafiki yako. Mmekuwa na wakati mzuri, lakini unaanza kuikumbuka familia yako mwenyewe. Kisha baba yako anakutumia ujumbe mfupi kuona mambo yanaendaje—ndicho hasa ulichohitaji kuhisi unapendwa na kukumbukwa.

Maisha Ulimwenguni kwa kiasi kidogo ni kama hivyo. Mungu hatutumii ujumbe mfupi, lakini tupo mbali na nyumbani kwetu mbinguni, hivyo njia moja ambayo Baba wa Mbinguni huwasilisha upendo Wake kwetu ni kwa kuwatuma manabii.

Kipindi cha Mwongozo wa Mungu

Picha
prophets called of God

Vielelezo na Ben Simonsen

Manabii huongoza kile kinachoitwa vipindi vya mwongozo wa Mungu, vipindi vya nyakati ambapo (1) Mungu anakuwa na angalau kiongozi mmoja wa ukuhani aliyepewa mamlaka duniani na (2) kiongozi huyu, nabii, hujifunza kuhusu mpango wa wokovu moja kwa moja kutoka kwa Mungu. Nabii kisha hufundisha, au hutoa, injili kwa watu.

Shukrani kwa maandiko, tunajua kuhusu vipindi vingi vya mwongozo wa Mungu. Baadhi ya vile muhimu ilikuwa ni cha Adamu, Henoko, Nuhu, Ibrahamu, Musa, Yesu Kristo na Joseph Smith. Bwana alianzisha kipindi cha mwongozo wa Mungu kupitia kila mmoja wa manabii hawa.

Ukengeufu

Picha
apostasy cycle

Ukengeufu=uovu. Wakati mtu binafsi au kikundi wanapogeuka kutoka kwenye ukweli wa injili ya Yesu Kristo, wanawakataa manabii, na kuanguka katika dhambi, wanakuwa katika ukengeufu.

Je, ni kwa Jinsi gani Ukengeufu Hutokea?

Mungu humwita nabii, anayefundisha injili ya kweli ya Yesu Kristo.

Watu wanaofuata mafundisho ya nabii wanabarikiwa.

Baadhi ya watu wanakuwa wenye kiburi na kuwakataa manabii.

Bwana mara nyingi humwondoa nabii Wake kutoka kwa watu ambao wanakataa kanuni za injili.

Muda muafaka unapofika, Mungu humwita nabii mpya ili kurejesha ukweli, ukuhani, na Kanisa.

Urejesho

Picha
restoration

Urejesho ni tendo la kurudisha kitu katika hali yake halisi. Siyo kutengeneza upya, ambako ni kubadilisha kitu kilichopo na kutengeneza kitu kipya. Kwa mfano, kama ukitaka kurejesha nyumba ya zamani, utaijenga upya kwa mpangilio ule ule halisi iliyokuwa nao. Unaweza kuhitaji kuongeza sehemu mpya ya mekoni, lakini hapo utakuwa unabadilisha nyumba, siyo kuirejesha.

Injili ya Yesu Kristo ilihitajika kurejeshwa kwa sababu ilipotea wakati wa Ukengeufu Mkuu. Watu walikuwa wameishi kwa karne nyingi bila Kanisa la kweli. Hivyo Bwana alirejesha Kanisa Lake na injili kupitia Joseph Smith, kama vile manabii wa kale walivyotoa unabii (ona Isaya 2:1–3; 29:13–14; Matendo ya Mitume 3:19–21; Ufunuo 14:6–7; 2 Nefi 3:3–15).

Injili ya kweli ya Yesu Kristo iko hapa daima—kwa hivyo wewe utakaa nayo daima? Japokuwa ulimwengu unakua mwovu zaidi na zaidi, Kanisa la Yesu Kristo litabaki hadi mwisho.

Una uchaguzi wa kufanya—uchaguzi ule ule ambao umewapata wanadamu tangu mwanzo wa nyakati: je, utamfuata nabii? Ukimfuata nabii, utabarikiwa na kuwa na Roho ili kukuongoza.

Adamu

Adamu alikuwa mwanzilishi wa kweli: yeye alikuwa mtu wa kwanza duniani na nabii wa kwanza! Aliifundisha familia yake injili, lakini hata mwanzo, wengi “walitafuta ushauri wao wenyewe gizani” na kuukataa ukweli (Musa 6:28).

Henoko

Picha
city taken up to heaven

Je, umewahi kusikia juu ya mji wote kuchukuliwa kwenda mbinguni? Vema, mji wa Sayuni—ulianzishwa na Henoko—ulikuwa wa haki zaidi kwamba watu wake walienda kukaa na Mungu (ona Musa 7:23).

Nuhu

Picha
noahs ark

Unajua kuhusu safina ya Nuhu. Watu wanane tu—familia ya Nuhu—walinusurika na Mafuriko kwa sababu walisikiliza maonyo ya Nuhu (ona Mwanzo 7; Musa 8). Lakini ulijua kwamba alipokea ukuhani alipokuwa na umri wa miaka 10 (ona M&M 107:52) na kwamba “mapandikizi ya watu … walimtafuta Nuhu ili wamtoe uhai wake”? Musa 8:18.

Ibrahimu

Picha
abraham

Ibrahimu alikuwa karibu atolewe kafara na makuhani waovu, lakini malaika alimuokoa (ona Ibrahimu 1). Alipata baadhi ya ufunuo wa kupendeza, ikijumuisha ono la maisha kabla ya kuja duniani. Waumini wa Kanisa ni uzao wake, na agano la Ibrahimu limepewa jina kutoka kwake. (Ona Ibrahimu 2–5.)

Musa

Picha
moses

Musa aliwaongoza Waisraeli kutoka Misri na kuwasaidia kupata uhuru wao. Yeye “alitafuta kwa bidii kuwatakasa watu wake ili kwamba wauone uso wa Mungu; lakini walifanya mioyo yao kuwa migumu na hawakuweza kustahimili uwepo wake” (M&M 84:23–24). Hakika, kwa sababu ya ukengeufu wao, walitangatanga nyikani kwa miaka 40!

Yesu Kristo

Picha
Jesus Christ

Siyo tu kwamba Yesu Kristo alifundisha injili na kufanya miujiza mingi, lakini pia alianzisha Kanisa Lake duniani. Yeye alilipia adhabu ya dhambi zetu na alisulubiwa na kufufuka ili kutuwezesha sisi kushinda kifo cha kiroho na cha kimwili. Yeye ndiye kichwa cha Kanisa Lake leo, na Yeye na Baba wa Mbinguni ni chanzo cha mamlaka ya ukuhani.

Ukengeufu Mkuu

Picha
the great apostasy

Baada ya Ufufuko wa Mwokozi, Mitume Wake na viongozi wengine wa Kanisa walijaribu kuieneza injili, lakini watu walikataa mafundisho yao na hata kuwaua Mitume wengi. Kwa sababu ya uovu wa watu, utimilifu wa injili ulipotea duniani. Ulimwengu uliangukia kwenye giza la kiroho (ona Isaya 60:2).

  • Kwa zaidi ya miaka 1,000, watu hawakuweza kupata ibada za wokovu, baraka za hekaluni, au mwongozo wa nabii.

  • Ukweli wenye thamani ulipotea kutoka kwenye Biblia.

  • Dhana za uongo zilifundishwa kuhusu ukweli juu ya asili ya Mungu.

  • Baadhi ya ibada za wokovu zilibadilishwa au kufundishwa visivyo sahihi (ona Isaya 24:5).

  • Ukengeufu huu hatimaye ulileta kuanzishwa kwa makanisa mengi.

Kutengeneza Upya

Picha
reformation

Wakati wa Ukengeufu Mkuu, baadhi ya watu wenye mawazo ya-kidini huko Ulaya waligundua kwamba injili ya Yesu Kristo haikuwa ikifundishwa kwa usahihi. Watengenezaji upya hawa hawakuwa manabii, lakini walifanya kwa kadri ya uwezo wao kufundisha ukweli jinsi walivyouelewa. Walisaidia kufanya Biblia ipatikane kwa watu wengi zaidi. Wengi walipigania uhuru wa dini na kufungua njia kwa ajili ya Urejesho wa injili.

Joseph Smith

Picha
joseph smith

Hivyo utimilifu wa injili ulikuwa umepotea milele? La! Mungu alifunua ukweli muhimu kwa Joseph Smith tena. Wajumbe wa Mbinguni walirejesha kwake funguo zote muhimu za ukuhani (ona M&M 27:8–13; 110; 128:18–21), zikifanya hiki kuwa “kipindi cha mwongozo wa Mungu cha utimilifu wa nyakati” (M&M 138:48). Pia kinajulikana kama siku za mwisho kwa sababu ni kipindi cha mwisho cha mwongozo wa Mungu kabla ya Ujio wa Pili wa Yesu Kristo.

Urejesho

Je, unajua? WEWE una baraka za Urejesho. Ndiyo, wewe!

  • Kanisa la Yesu Kristo lilirejeshwa likiwa na nabii na mitume ili kuliongoza.

  • Kitabu cha Mormoni, Mafundisho na Maagano, Lulu ya Thamani Kuu, na ufunuo mwingine wa kisasa vilirejesha ukweli wa thamani uliokuwa umepotea (ona 2 Nefi 27).

  • Joseph Smith alipokea Ukuhani wa Haruni kutoka kwa Yohana Mbatizaji (ona M&M13) na Ukuhani wa Melkizedeki kutoka kwa Petro, Yakobo, na Yohana (ona M&M 128:20).

  • Wenye ukuhani waliopewa mamlaka hufanya ibada za wokovu kwa usahihi.

  • Na tunajua kwamba ukweli kamwe hautaweza kupotea kwa njia ya ukengeufu tena (ona Danieli 2:44).