2018
Ninawezaje Kurejesha Kujifunza Maandiko Kwangu?
April 2018


Ninawezaje Kurejesha Kujifunza Maandiko Kwangu?

Sarah Keenan

Utah, Marekani

Picha
woman sitting at a desk

Kielelezo na Bradley Clark

Nilikuwa nimerudi nyumbani kutoka misheni yangu kwa miezi mitatu tu wakati nilipoanza kutatizika na kusoma maandiko.

Nilikuwa nikisoma maandiko kila siku nilipokuwa misheni na kuahidi kuendelea nitakaporudi nyumbani. Lakini kadiri muda ulivyokwenda, mambo yalionekana kuingilia kati. Nilikuwa aidha na kazi nyingi za nyumbani, nilikuwa nafanya kazi sana, au nilikuwa tu nimechoka sana. Kwa kila kisingizio, usomaji wangu wa maandiko ulififia mpaka nikawa sisomi kabisa.

Nilifungua Kitabu cha Mormoni usiku mmoja na kupanga kusoma mstari mmoja tu. Mstari niliosoma ulinikumbusha kwamba maandiko yana “neno la kupendeza la Mungu, ndio, neno ambalo linaponya nafsi iliyojeruhiwa” (Yakobo 2:8).

Nilitafakari mstari huu na kugundua matokeo hasi ambayo kuacha kusoma maandiko kuliniletea. Nilijihisi mwenye msongo wa mawazo shuleni, kutojali zaidi kanisani, na aliye mbali zaidi na Mungu. Nafsi yangu ilihitaji neno la kuponya la Mungu lililopatikana ndani ya maandiko. Nilijua nilihitaji kutambua vipaumbele vyangu.

Niliwageukia rafiki zangu, familia, na viongozi wa Kanisa kuuliza mapendekezo ya kurudisha nguvu ya kujifunza maandiko kwangu. Nilipata mambo matatu yenye msaada.

Kwanza, niligundua kwamba kujifunza maandiko usiku haikuwa na matokeo mazuri kwangu. Kujifunza asubuhi kuliniruhusu kutafakari kwa siku nzima mafundisho na kanuni nilizokuwa nimesoma asubuhi.

Pili, tumefunzwa kusoma maandiko na familia zetu, lakini kwa kuwa nilikuwa chuoni na mbali na familia yangu, nilianza kusoma maandiko na wenza wa chumbani na marafiki. Hii ilinisaidia kuwa mwajibikaji, na ilichochea majadiliano makubwa ya injili.

Tatu, nilianza kuandika ushawishi na mawazo niliyopokea wakati wa kujifunza maandiko. Hii ilinisaidia kuzingatia katika kile nilichokuwa nikisoma na kunisaidia kuitambua zaidi sauti ya Roho.

Mara kujifunza maandiko kukuwa kipaumbele katika maisha yangu tena, nilijiona kwamba nina muda mwingi zaidi na nguvu nyingi zaidi kwa ajili ya kukamilisha kila kitu nilichohitaji kukifanya. Muhimu zaidi, niliusikia ukaribu na Mungu tena kadiri nilivyosoma na kutafakari maandiko. Sasa ninapotumia muda katika maandiko, Ninahisi amani na kupata uponyaji kwa nafsi yangu.