Mkutano Mkuu
Zawadi Nzuri Sana ya Mwana
Mkutano Mkuu wa Oktoba 2020


Zawadi Nzuri Sana ya Mwana

Kupitia Yesu Kristo, tunaweza kuepuka uchungu tunaostahili wa kuanguka kwetu kimaadili na kushinda uchungu tusiostahili wa taabu zetu za maisha ya duniani.

Wakati nikisoma Kitabu cha Mormoni kwa ajili ya somo la Njoo, Unifuate majira yaliyopita ya joto, nilishangazwa na ripoti ya Alma kwamba mara alipokuwa na ufahamu kamili wa dhambi zake, hakungekuwa na “chochote kilichokuwa kikali vile na kichungu vile ulivyokuwa uchungu [wake].” 1 Ninakiri, maongezi ya uchungu mkali yalibaki akilini mwangu kwa namna moja ni kutokana na vita yangu wiki hiyo ya jiwe la figo lenye ukubwa wa milimita saba. Kamwe hakuna mtu yeyote amewahi kupitia “vitu hivyo vikubwa” wakati kitu hicho “kidogo na rahisi” “kilipotendeka.” 2

Lugha ya Alma pia ilichukua umakini wangu kwa sababu neno kikali sana katika tafsiri ya Kiingereza ya Kitabu cha Mormoni, kiuasilia huelezea vitu vya uzuri wa kipekee au utukufu usiolinganishwa. Kwa mfano, Joseph Smith alikumbuka kwama malaika Moroni alivaa joho “jeupe sana,” “weupe uliopita kitu chochote cha kidunia [alichowahi] kukiona.” 3 Lakini pia neno hilo linaweza kumaanisha ukali uliopitiliza hata kwa vitu vinavyoogopesha. Kwa hiyo Alma pamoja na kamusi nyingi hutoa maana ya maumivu makali kama “kuteswa,” “kuhuzunishwa,” na “kuogopeshwa” kwa “kiwango cha juu sana.” 4

Taswira ya Alma inaakisi uhalisia wa busara kwamba kwa kiwango fulani, mateso makali ya hatia ya kila dhambi tunayoitenda lazima yahisiwe. Haki inahitaji hilo, na Mungu Mwenyewe hawezi kulibadili. 5 Wakati Alma alipokumbuka dhambi zake “zote”—hasa zile zilizoharibu imani za wengine—mateso yake kiuhalisia yalikuwa yasiyovumilika, na dhana ya kusimama mbele za Mungu ilijaza nafsi yake na “hofu kuu isiyoelezeka.” Alitamani “angeangamizwa vyote nafsi na mwili.” 6

Hata hivyo, Alma alisema kila kitu kilianza kubadilika mara tu “alipokumbuka kuhusu” utabiri wa “kuja kwa mmoja aitwaye Yesu Kristo … kulipia dhambi za ulimwengu” na “alilia ndani ya moyo [wake]: Ee Yesu, wewe Mwana wa Mungu, nihurumie.” Kwa dhana hiyo moja na ombi hilo moja, Alma alijazwa na shangwe “ya ajabu” “kama vile ulivyokuwa uchungu [wake].” 7

Kamwe hatupaswi kusahau kuwa lengo hasa la toba ni kuondoa baadhi ya taabu na kuzibadili kuwa furaha kamili. Asante kwa “wema wake mwingi,” 8 mara tu tunaposonga kwa Kristo—tukionyesha imani Kwake na badiliko la kweli la moyo—uzito wa kuumiza wa dhambi zetu utaanza kuhama kutoka migongoni mwetu na kuhamia Kwake. Hii inawezekana kwa sababu Yeye asiye mdhambi aliteseka “maumivu yasiyo na mwisho na yasiyoongeleka” 9 ya kila dhambi ya ulimwengu Aliouumba, kwa ajili ya vyote Alivyoviumba—mateso machungu sana, damu ikabubujika toka katika kila kinyweleo. Kutoka katika uzoefu binafsi, Mwokozi hivyo anatuonya, katika maandiko ya leo, kwamba hatuna uelewa wa jinsi ya “ukali” wa “mateso” yetu yatakavyokuwa kama hatutatubu. Lakini kwa wema usiopimika Yeye pia anafafanua kwamba “Mimi, Mungu, nimeteseka mambo haya kwa ajili ya wote, ili kwamba wasipate kuteseka kama watatubu” 10 —toba inayoturuhusu sisi “kupata” “shangwe kuu” ambayo Alma aliipata. 11 Kwa fundisho hili pekee, “nashangaa sana.” 12 Na bado, kwa mshangao, Kristo alitoa zaidi.

Wakati mwingine maumivu makali huja sio kutokana na dhambi bali makosa ya uaminifu, matendo ya wengine, au nguvu zinazotuzidi uwezo. Katika nyakati hizi, unaweza kulia kama mtunga zaburi wa haki:

“ Moyo wangu unaumia ndani yangu, Na hofu za mauti zimeniangukia.

“… Na hofu kubwa imenifunikiza.

“… Ningekuwa na mbawa kama njiwa, Ningerukia mbali na kustarehe.” 13

Wanasayansi wa madawa, watoa ushauri wabobezi au msaada wa kisheria vinaweza kusaidia kuondoa mateso hayo. Lakini kumbuka, vipawa vyote vyema—ikiwemo hivi—vinatoka kwa Mwokozi. 14 Bila kujali visababishi vya maumivu yetu makali au maumivu ya moyo, chanzo kikuu cha msaada ni kile kile: Yesu Kristo. Yeye peke yake ana nguvu kamili na faraja ya kuponya ili kusahihisha kila kosa, kurekebisha kila baya, kuweka sawa kila pungufu, kuponya kila jeraha, na kutoa kila baraka iliyochelewa. Kama mashuhuda wa kale, ninashuhudia kwamba “hamna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika mambo yetu ya udhaifu” 15 ila tu Mkombozi mwenye upendo aliyeacha kiti Chake huko juu na kwenda “kuteseka maumivu na masumbuko na majaribio ya kila aina …, ili ajue … jinsi ya kuwasaidia watu wake.” 16

Kwa yeyote mwenye maumivu makali sana au ya kipekee sana kwamba unahisi hakuna anayeweza kuyakubali, unaweza kuwa sahihi. Kunaweza kusiwepo mwanafamilia, rafiki, au kiongozi wa ukuhani—hata wawe na hisia gani na kumaanisha kwao—nani anajua hasa kile unachokihisi au ana maneno halisi ya kukusaidia kupona. Lakini tambua hili: kuna Mmoja anayeelewa vyema kile unachopitia, ambaye ni “mkuu kupita ulimwengu wote,” 17 na ambaye “awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote [sisi] tuyaombayo au tuyawazayo.” 18 Mchakato utajifunua katika njia Yake na katika wakati Wake, bali Kristo yu tayari siku zote kutibu kila kitu na kila kipengele cha uchungu wako.

Unapomruhusu Yeye kufanya hivyo, utagundua kwamba maumivu yako hayakuwa bure. Ukiongelea mashujaa wengi wakubwa wa Biblia na mateso yao, mtume Paulo alisema kwamba “Mungu … alitangulia kuwawekea vitu vilivyo bora kupitia mateso, kwani bila mateso wao wasingeweza kukamilishwa.” 19 Unaona, uhalisia wa Mungu na lengo la uwepo wetu hapa duniani ni furaha, 20 lakini hatuwezi kuwa viumbe vikamilifu vyenye furaha bila uzoefu wa kutujaribu, wakati mwingine unaochoma sana. Paulo anasema kwamba hata Mwokozi mwenyewe alifanywa kuwa “mkamilifu [au mzima] milele kupitia mateso.” 21 Kwa hiyo jilinde dhidi ya mnong’ono wa kishetani kwamba kama wewe ni mtu mwema, utaepuka mateso hayo.

Unapaswa pia kuepuka uongo kwamba mateso yako kwa kiasi fulani yanapendekeza kwamba usimame nje ya mduara wa wateule, ambao huonekana kuteleza kutoka hali moja ya baraka kwenda nyingine. Badala yake, jione mwenyewe kama Yohana mfunuzi alivyokuona katika ufunuo wake usio na kifani wa siku za mwisho. Kwani Yohana aliona “mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha, [ambao] wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo, wamevikwa mavazi meupe, … [huku] wakilia kwa sauti kuu wakisema, Wokovu una Mungu wetu.” 22

Alipoulizwa “Je! watu hawa waliovikwa mavazi meupe ni akina nani? Na wametoka wapi?” Yohana alipokea jibu: “Hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu, nao wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” 23

Akina kaka na dada, kuteseka kwa haki hutusaidia kufuzu kuwa, na sio kututofautisha na, wateule wa Mungu. Na hufanya ahadi zao kuwa zako. Kama Yohana alivyotangaza “Hawataona njaa tena, wala hawataona kiu tena; wala jua [halitakupiga], wala joto lolote. Kwa maana huyo Mwana-Kondoo aliye katikati ya kiti cha enzi [atakuchunga], naye [atakuongoza] kwenye chemichemi za maji yenye uhai: na Mungu atayafuta machozi yote katika macho [yako].” 24

“wala mauti haitakuwapo tena, wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena.” 25

Ninashuhudia kwenu kwamba kupitia wema mkuu wa Yesu Kristo na Upatanisho wake usio na mwisho, tunaweza kuepuka uchungu tunaostahili wa kuanguka kwetu kimaadili na kushinda uchungu tusiostahili wa taabu zetu za maisha ya duniani. Chini ya uelekezi wake, kudra yako takatifu ni moja ya shangwe isiyofananishwa na ya kitukufu—shangwe ya kina sana na ya kipekee kwako, “majivu” yako yatakuwa uzuri “uzidio chochote cha ulimwengu.” 26 Kwamba uweze kujaribu shangwe hii sasa na kujazwa nayo milele, ninakualika kufanya kile Alma alikifanya: acha mawazo yako yajikite kwenye zawadi nzuri sana ya Mwana wa Mungu kama ilivyofunuliwa kupitia injili Yake, katika hili kanisa Lake la Kweli na hai. Katika Jina la Yesu Kristo, amina.